Longido ni maarufu kwa ng’ombe wa kimaasai wenye sifa bora za nyama.
Uwekezaji kwenye feedlots utasaidia kunenepesha ng’ombe kabla ya kuuza sokoni au kusafirisha nje ya nchi.
Soko: Kenya (Namanga OSBP), Dar es Salaam, na nchi za Kati ya Afrika.
Uhitaji wa machinjio ya kisasa na kiwanda kidogo cha nyama (beef processing) kwa ajili ya nyama safi, sausage, minofu na nyama iliyokaushwa.
Faida: kuongeza thamani ya mifugo, ajira kwa jamii, na upatikanaji wa bidhaa za nyama zenye viwango vya kimataifa.
Ingawa jamii ya kimaasai hutegemea maziwa, hakuna viwanda vya kusindika maziwa kwa kiwango kikubwa.
Uwekezaji unaweza kuanzisha:
Kiwanda cha pasteurization
Utengenezaji wa mtindi, siagi, jibini
Fursa ya masoko: shule, mahoteli, Namanga na Arusha.
Longido ina idadi kubwa ya ng’ombe, mbuzi na kondoo → ngozi ni nyingi lakini zinapotea bila kuchakatwa.
Uwekezaji:
Depots za kukusanya ngozi
Kiwanda cha kusindika ngozi (leather processing) kwa bidhaa kama viatu, mikanda, mifuko.
Tatizo kubwa: ukame mara kwa mara → upungufu wa malisho.
Fursa: kulima nyasi bora (Rhodes, Chloris, Alfalfa) na kuzisindika kuwa hay bales au pellets.
Soko: wafugaji wa Longido na wilaya jirani.
Uwekezaji kwenye veterinary centres na maduka ya dawa za mifugo.
Utoaji wa huduma: chanjo, tiba, huduma za kuzuia magonjwa, na ushauri wa afya ya mifugo.
Ujenzi wa minada ya kisasa yenye mizani za kidijitali, mabanda ya mifugo, na huduma za daktari wa mifugo.
Eneo la Namanga lina nafasi kubwa kwa sababu ni lango la kuuza mifugo Kenya.
Kuna ongezeko la ufugaji wa ngamia (maziwa ya ngamia yana soko kubwa kimataifa).
Nafasi ya kuwekeza kwenye mashamba ya ngamia na kusindika maziwa yake.
Pia, poultry farming kwa mayai na nyama – kuongeza lishe na kipato cha jamii.
NB; Kwa nini kuwekeza kwenye mifugo Longido?
Wilaya ina zaidi ya ng’ombe, mbuzi, kondoo na ngamia kwa wingi.
Soko la karibu: Kenya kupitia Namanga OSBP (biashara ya kimataifa).
Hali ya hewa na utamaduni: Jamii ya Wamaasai imejikita kwenye mifugo → kuna uhakika wa upatikanaji wa malighafi.
Kwa Mawasiliano zaidi fika
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Longido,
AU
Piga Simu 0782749201 - Afisa Mifugo Wilaya
Arusha- Namanga Road, Longido Town
Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha
Telephone: +255 272 970 793/ 94
Mobile: 0756395889
Email: ded@longidodc.go.tz
Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.