• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

COMPASSION NA SERIKALI WAUNGANA KUMWEZESHA MTOTO WA KIKE NAMANGA

Posted on: October 13th, 2025

Na.HAPPINESS NSELU


Ofisi ya Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Longido kwa kushirikiana na Shirika la Compassion linalotoa huduma za malezi kwa watoto na vijana kupitia Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Namanga, wameendelea kutoa elimu kwa watoto wa kike ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani, ambayo huadhimishwa kila mwaka Oktoba 11.


Tukio hilo limefanyika Oktoba 13 katika kituo cha Compassion kilichopo Namanga, chini ya uratibu wa Mratibu wa kituo hicho, Elihuruma Pendael, likihusisha wasichana kutoka maeneo mbalimbali ya kata hiyo.


Afisa Maendeleo ya Jamii, Bi Monica Wambura, Bi Elmina Thadei na Bi Scolastica Kimario ndio waliongoza utoaji wa elimu hiyo kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Compassion, wakilenga kumjengea mtoto wa kike uelewa wa haki zake za msingi, ujasiri wa kujilinda dhidi ya ukatili wa kijinsia na umuhimu wa elimu katika kutimiza malengo yao ya maisha.


Aidha, wasichana walioshiriki walipewa taulo za kike kama sehemu ya kampeni ya kuwasaidia kutunza afya ya uzazi na kuondoa changamoto zinazoweza kuwazuia kuhudhuria masomo kwa ufanisi.

Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Mimi ni Msichana, Kinara wa Mabadiliko kwa Tanzania Tuitakayo 2050”, ikisisitiza jukumu la jamii katika kumwezesha mtoto wa kike kupata elimu bora, ulinzi na fursa sawa za maendeleo.


Akizungumza katika tukio hilo, Bi Monica Wambura alisema elimu kwa mtoto wa kike ni msingi wa ustawi wa taifa, hivyo jamii inapaswa kumpa nafasi ya kujifunza, kujitambua na kutimiza ndoto zake bila vizuizi.

Kwa upande wake, Mratibu wa Kituo cha Compassion Namanga, Elihuruma Pendael, alisema shirika hilo litaendelea kushirikiana na serikali katika jitihada za kumlinda na kumjengea mtoto wa kike uwezo kupitia elimu na malezi chanya, ili kufikia Tanzania yenye usawa wa kijinsia na maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2050

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • WWF YAWANOA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU SERA YA UTUNZAJI MAZINGIRA LONGIDO

    October 15, 2025
  • COMPASSION NA SERIKALI WAUNGANA KUMWEZESHA MTOTO WA KIKE NAMANGA

    October 13, 2025
  • SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S YAUNGA MKONO MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA, YAFUNGA MFUMO WA GESI

    October 14, 2025
  • SERIKALI YAAHIDI KUMALIZA KERO YA MAJI SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S IFIKAPO JANUARI 2026

    October 14, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.