• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO IMEFANYA KIKAO KAZI CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE .

Posted on: November 11th, 2024

Na Happiness Nselu



Kikao kazi cha tathmini ya lishe kilichofanyika leo katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Longido, kikiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Salum Kalli.


Katika kikao hicho, Mheshimiwa Kalli alisisitiza umuhimu wa lishe bora kwa jamii, akieleza kwamba afya ya mama na mtoto inategemea sana mlo kamili na usawa. Alisisitiza pia kuwa, ni muhimu kwa kina baba kushiriki kikamilifu katika kujenga afya ya familia zao, hususan katika kuhakikisha mlo bora kwa wake zao na watoto wao.


Afisa Lishe wa Wilaya Bi. Adelina Kahija alisoma tathmini ya lishe katika wilaya, akionyesha mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto zinazohitaji kushughulikiwa ili kuboresha lishe kwa jamii. Aliwahimiza viongozi na wananchi kuongeza jitihada za kutoa elimu zaidi kuhusu mlo bora, ili kupambana na utapiamlo na magonjwa yanayotokana na lishe duni.


Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Deoniz Mathew Majani, alitoa shukrani kwa wajumbe wa kikao hicho kwa kazi yao ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa mlo kamili.


Alisisitiza kuwa jamii inahitaji kuendelea kuwa na uelewa wa juu kuhusu lishe bora na akasema kwamba ni muda sasa wa kuhamasisha jamii kuhusu hatari ya wamama kujifungulia nyumbani, na umuhimu wa kujifungulia katika vituo vya afya kwa usalama wa mama na mtoto.


Aidha, Dkt. Deoniz Mathew Majani alizungumza kuhusu huduma ya "M-Mama" inayotolewa na Serikali ambayo ni huduma ya usafirishaji wa wamama wajawazito na watoto wenye mahitaji maalum kutoka vijijini hadi vituo vya afya.


Alisisitiza kuwa huduma hii ni muhimu kwa afya ya mama na mtoto, na alitoa wito kwa watendaji wa kaya na vijiji kuwa na madereva jamii watakaorahisisha upatikanaji wa huduma hii kwa haraka na ufanisi. Alisema kuwa ni muhimu kuhakikisha kwamba huduma za usafiri zipo karibu na wananchi, ili kuepusha vifo vya uzazi na madhara yanayoweza kutokea kutokana na ucheleweshaji wa huduma za afya.


Kikao hicho kilihudhuriwa na watumishi wa Halmashauri pamoja na  watendaji wa serikali, na kililenga kuimarisha ushirikiano wa pamoja katika kuhakikisha wilaya ya Longido inakuwa na lishe bora na huduma bora za afya kwa wote.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.