• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Posted on: August 7th, 2025

Na Happiness Nselu

 Halmashauri ya Wilaya ya Longido imeadhimisha Wiki ya Unyonyeshaji tarehe 7 Agosti 2025 kwa mafanikio makubwa kupitia sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Eorendeke, Kata ya Kimokouwa, na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi, watoa huduma za afya na viongozi wa jamii.


Maadhimisho hayo, yaliyolenga kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa watoto wachanga na lishe bora kwa familia, yalipambwa na uwepo wa Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli, ambaye alikuwa mgeni rasmi.


Mganga Mkuu wa Wilaya, Dk. Methew Majani, akisoma risala rasmi, alieleza dhamira ya halmashauri katika kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto. Alisisitiza kuwa unyonyeshaji sahihi unalinda afya ya watoto wachanga, unapunguza vifo vya watoto na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla.


Afisa Lishe wa Wilaya, Bi Adelina Kahija, alitoa elimu kwa kina kwa kina mama na walezi kuhusu umuhimu wa kunyonyesha ndani ya saa moja baada ya kujifungua, unyonyeshaji wa pekee kwa miezi sita ya mwanzo, na kuhakikisha familia inapata mlo kamili wenye virutubisho muhimu.


“Tunataka kila kaya hapa Longido ifahamu kuwa unyonyeshaji ni msingi wa kizazi chenye afya, na lishe bora ni jukumu la familia nzima,” alisema, akihimiza wanaume kushirikiana na wake zao katika jukumu hilo.


Sherehe hizo zilipambwa na burudani kutoka kikundi cha muziki cha ACE Group, kilichotumbuiza kwa nyimbo zenye ujumbe wa kuhamasisha unyonyeshaji, malezi bora ya mama na mtoto, pamoja na ulaji wa chakula chenye virutubisho.

Mheshimiwa Kalli alisifu waandaaji na wadau kwa jitihada zao, akiwataka wananchi kuyatumia mafunzo yaliyotolewa. “Mama mwenye afya analea mtoto mwenye afya, na mtoto mwenye afya anajenga taifa imara,” alisisitiza.


Wiki ya Unyonyeshaji huadhimishwa duniani kote kila mwaka katika wiki ya kwanza ya Agosti, huku kaulimbiu ya mwaka huu ikisema "THAMINI UNYONYESHAJI ;WEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA MAMA NA MTOTO".


@ortamisemi@wizara_afyatz@rc_mkoa_arusha@ikulu_mawasilian

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.