ARUSHA, Mei 27, 2025 – Wilaya ya Longido leo imepeleka rasmi timu yake ya michezo ya UMITASHUMTA kuelekea Mkoani Arusha kwa ajili ya kushiriki mashindano ya ngazi ya mkoa yatakayofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 31 Mei 2025 katika viwanja vya Shule ya Msingi Ilboru.
Timu hiyo yenye wanafunzi 83 kutoka shule mbalimbali za msingi Longido, inatarajiwa kushiriki katika michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu (wavulana na wasichana), mpira wa wavu (wavulana), handball (wavulana na wasichana), netball, riadha,pamoja na Kizazi Kipya, ambayo inalenga kukuza vipaji vya sanaa kwa watoto.
Akizungumza wakati wa kuwaaga wachezaji hao, Afisa Elimu Michezo wa Wilaya ya Longido, Bi. , aliwataka Jesca Bosco Rwezaura wanafunzi hao kuwa mabalozi wema wa wilaya yao kwa kuzingatia nidhamu, ushindani wa haki, na mshikamano. “Mnakwenda kuiwakilisha Longido, mnapaswa kuonyesha uzalendo, nidhamu na kushirikiana kama timu. Mafanikio yenu ni fahari kwa wilaya nzima,” alisema Leikoi.
Timu hiyo inaongozwa na jumla ya walimu wa michezo sita (6)waliobobea katika michezo husika, ambao watasimamia ustawi wa wanafunzi wakati wote wa mashindano.
Mashindano ya UMITASHUMTA ni sehemu ya kalenda ya kitaifa ya michezo kwa shule za msingi na hutoa fursa kwa wanafunzi kuonyesha vipaji vyao na kuandaliwa kwa mashindano ya kitaifa.
Wilaya ya Longido inatarajia kufanya vizuri katika mashindano hayo kufuatia maandalizi mazuri na hamasa kubwa kutoka kwa walimu, wazazi na viongozi wa wilaya.
Arusha- Namanga Road, Longido Town
Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha
Telephone: 027-2539603
Mobile: 0756395889
Email: ded@longidodc.go.tz
Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM