• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KATIBU MKUU TAMISEMI AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI LONGIDO

Posted on: September 13th, 2019

Katibu mkuu  ofisi ya Raisi tawala za mikoa na serikali za mitaa Tamisemi Mhandisi.Joseph Nyamhanga akiambatana na katibu tawala mkoa Arusha na secretariati ya mkoa leo tarehe 13-09-2019 akiwa katika halmashauri ya wilaya ya Longido amefanya ziara ya kutembelea na kujionea  miradi mbalimbali ya maendeleo yaliyopo wilayani .Mhandisi Nyamhanga ametembelea kiwanda kidogo cha mikate kinacho julikana kwa jina la BLESSING BEKARY, ambapo waliweza kumueleza Katibu mkuu TAMISEMI kuwa walianza mradi wao kwa kiwango cha fedha taslim milioni kumi walio chukua kama mkopo kutoka ofisi ya maendeleo ya jamii Halmashauri ya wilaya Longido akieleza afisa maendeleo ya Jamii Bi. Grace kuwa waliweza kutoa zaidi ya milioni mia moja thelathini kwa ajili ya  vikundi ikiwa asilimia 6% ni kwa ajili ya wakina mama na kikundi cha vijana 2% pamoja na walemavu 2%, Kikundi hichi kilinufaika kwa ujio wa kiongozi huyo kwani aliweza kununua mikate miamoja  ambayo aliitoa zawadi pamoja na mbuzi kwa kituo cha watoto yatima Namanga. Pia alitembelea vituo vya afya cha Eworendeke pamoja na kutembelea miradi inayoendelea ikiwemo hospitali ya wilaya, barabara ya kiwango cha lamiyenye urefu wa kilomita moja kutoka kituo cha polisi Longido hadi zahanati ya Longido na kutembelea kikundi cha walemavu kinachojulikana kwa jina la OSILIGI kilichopo kata ya kimokouwa wilayani Longido katibu mkuu TAMISEMI aliweza kuwaunga mkono kwa kununua mbuzi moja wapo wa mbuzi wanao nenepeshwa na kikundi hicho kwa shilingi Laki moja (100,000/=)

Katika ziara hiyo katibu mkuu ndugu Mhandisi Joseph Nyamhanga alipata fursa ya kufanya kikao kifupi na watumishi  wa Halmashauri ya wilaya wakiwemo wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri, taasisi za kiserikali tarura, maafisa taarafa na watendaji wa kata.

 Katika kikao hicho mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya  Longido Ndugu Jumaa Mhina alipata fursa ya kutoa taarifa ya miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo katika halmashauri pamoja na miradi mikakati takribani kumi ambayo ikikamilika itaongeza mapato ya halmashauri kufikia takribani bilioni sabini kwa mwaka.

 Pia mkurugenzi mtendaji ndugu Jumaa Mhina alisema Halmashauri imepiga hatua kubwa kwenye sekta mbalimbali ukilinganisha na miaka iliyopita mfano kwenye ukusanyaji mapato umeongezeka kutoka tsh milioni 400 mpaka tsh bilioni 2, sekta ya elimu imekuwa ya pili kimkoa na ya tano kitaifa kwenye mitihani ya kidato cha pili mwaka jana na watumishi wengi waliokuwa hawajathibitishwa kwenye idara na vitengo vyao sasa wamethibitishwa. Pia katika kikao hicho katibu tawala wilaya  ndugu Toba Nguvila alielezea changamoto ya gari la kufanyia patroo ndani ya Wilaya ya Longido yenye ukubwa wa kilomita 320 katibu mkuu TAMISEMI alijibu kuwa atalifanyia kazi kwa haraka kwani hili ni eneo la mpakani hivyo ni muhimu kuwa na gari hilo ili kulinda maliza raia na utorohwaji wa mifugo kuingia nchi  jirani.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM