• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ALIDHISHWA NA MIRADI ALIYOZINDUA WILAYANI LONGIDO.

Posted on: September 16th, 2018

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2018 Ndg. Charles.F.Kabeho alitembelea miradi sita ya maendeleo tarehe 15/09/2018 . Baadhi ya miradi imewekwa jiwe la msingi, kufunguliwa , kutembelewa na kuzinduliwa.Miradi hiyo kwa ujumla imegharimu serikali takriban Tsh. 2,892,288,316.00.

Miradi hiyo iliyozinduliwa na kuwekewa jiwe la Msingi na kutembelewa ipo katika sekta mbalimbali za utawala bora,Elimu,Afya,Maendeleo ya jamii,Kilimo na Maji.

Ndg .kabeho aliweka jiwe  la msingi katika ofisi ya kijiji ya Noondoto ujenzi uliogharimu kiasi cha Tsh.47,000,000/-.

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa pia amezindua madarasa matatu katika shule ya msingi kitumbeine ujenzi uliogharimu kiasi cha Tsh.53,450,000/-

Vile vile kiongozi wa mbio za mwenge  ameweka jiwe la msingi katika kituo cha afya Ketumbeine, mradi uliogharimia Tsh. 600,000,000/-

Ndg.Kabeho pia amezindua mradi wa maji kijiji cha mairowa wenye thamani ya Tsh.1,903,998,800.

Hata hivyo  Kabeho ameendelea kuifurahia miradi ya Longido na kuitolea mfano hata wakati wa kukabidhi mwenge huo kwa halmashauri ya Arusha.

Amesema nimeona ujenzi wa madarasa matatu yenye viwango yamejengwa kwa gharama ndogo ya milioni 53,000,000/- na mazingira yake ni magumu hata kusafirisha vifaa ,sasa nakuja huko nikiwa na picha ya Longido katika kutekeleza miradi ya maendeleo alimaliza ndg.Kabehe.

Ndg. Charles pia alitoa ujumbe wa mwenge uliosisitiza, wananchi katika sekta ya elimu kuendelea kutekeleza majukumu yao ya msingi kwa watoto wao. Serikali imeondoa michango na ada kwa shule za msingi na sekondari mpaka kidato cha nne. Wazazi wanapaswa kuwapa wanafunzi, sare za shule, madaftari, kalamu viatu na kuwapatia chakula wanapokuwa shuleni. 

Ndg. Kabeho amesema serikali inaendelea na mapambano dhidi ya ukimwi, imeendelea kusisitiza watu kujua afya zao. Mpango wa sasa ni kuomba wanaume kujitokeza kupima na kupata ushauri nasaha, wanaume wamekuwa wagumu mno kujitokeza kupima.

Ndg. Kabeho amesema serikali inaendelea na mapambano dhidi ya rushwa, rushwa ni adui wa  haki  ni vizuri kutoa taarifa kwa vyombo husika au kutumia namba 113 ambayo ni bure kwa mitandao yote. Ndg. Kabeho amesema serikali inaendelea na mapambano dhidi  ya malaria serikali inatoa vyandarua kwa kinamama wajawazito. Nivyema kujua matumizi sahihi ya vyandarua hivi.  

Ndg kabeho amesema serikali inaendelea na mapambano dhidi ya dawa za kulevya, ni vizuri wananchi wakaacha matumizi mabaya ya dawa za kulevya kwa sababu yanaongeza vitendo vya uhalifu na kurudisha maendeleo nyuma

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA PILI YA MAFUNZO YA WWF KWA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA LONGIDO

    October 16, 2025
  • WWF YAWANOA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU SERA YA UTUNZAJI MAZINGIRA LONGIDO

    October 15, 2025
  • COMPASSION NA SERIKALI WAUNGANA KUMWEZESHA MTOTO WA KIKE NAMANGA

    October 13, 2025
  • SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S YAUNGA MKONO MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA, YAFUNGA MFUMO WA GESI

    October 14, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.