• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

LONGIDO DC YAKUTANA NA WADAU KUWEKA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: January 6th, 2026

*Mkuu wa Wilaya kuanza ziara ya uhamasishaji kesho

NA ABRAHAM NTAMBARA

Halmashauri ya Wilaya ya Longido leo, Januari 6, 2026, imefanya kikao cha wadau wa Bima ya Afya kwa Wote kwa lengo la kuweka mikakati ya uhamasishaji kuelekea utekelezaji wa huduma hiyo, itakayozinduliwa rasmi hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. Samia aliyoitoa wakati wa kampeni, ya kuhakikisha kuwa ifikapo siku 100 tangu kuanza kwa awamu ya pili ya uongozi wake kuanzia Novemba 3, 2025 alipoapishwa, kila Mtanzania anakuwa na Bima ya Afya.

Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Longido, Katibu Tarafa wa Tarafa ya Longido, Bw. Alex Wambura, amesema kuwa kufanyika kwa kikao hicho kunadhihirisha kuanza rasmi kwa utekelezaji wa ahadi hiyo ya Rais kwa wananchi.

“Na kabla ya siku hizi 100 kuisha, tutahakikisha tunafika katika kata zote za Wilaya ya Longido kufanya uhamasishaji. Ratiba ya Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, Salum Kalli, inaanza kesho asubuhi kwa kufanya kikao Kimokouwa, ambapo moja ya ajenda kubwa kabisa itakuwa ni Bima ya Afya kwa Wote. Tunaamini kuwa kabla ya kutimia siku 100, tutakuwa tumemaliza kata zote 20 za Wilaya ya Longido,” amesema Bw. Mwita.

Ameongeza kuwa ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya itajumuisha Wakuu wa Idara na Vitengo vinavyohusika, Watendaji wa Kata pamoja na Wakuu wa Vituo vya Afya, ili kuhakikisha wananchi wa Longido wanapata taarifa sahihi na za kutosha kuhusu masuala ya Bima ya Afya kwa Wote.

Kwa upande wake, Afisa Uanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bw. Miraji Kisile, amesema kuwa huduma ya Bima ya Afya kwa Wote inatekelezwa chini ya Sheria Na. 13 ya mwaka 2023, Sura ya 365.

Amesema sheria hiyo inalenga kuweka mfumo wa kitaifa unaohakikisha kila mwananchi anakuwa na bima ya afya, ambapo makundi yote ya wananchi yanajumuishwa na hivyo kuondoa utaratibu wa kulipa fedha taslimu (cash) wakati wa kupata huduma za matibabu.

Bw. Miraji ameongeza kuwa lengo ni kuwa na mfumo madhubuti wa uchangiaji katika sekta ya afya, kwani uchangiaji wa mtu mmoja mmoja huleta changamoto. Ameeleza kuwa wananchi wenye uwezo watachangia, huku wale wasiojiweza wakilipiwa kupitia utaratibu maalum uliowekwa na Serikali.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya ya Longido, Dkt. Mathew Majani, amesema kikao hicho kimewakutanisha Watendaji wa Kata zote 20, Waganga Wafawidhi kutoka vituo vyote 38 vya kutolea huduma za afya, wajumbe wa Kamati ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT) pamoja na Kamati ya Huduma za Afya ya Wilaya (CHMT).

Amesema lengo la kikao hicho ni kuwahusisha wadau muhimu katika utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, na ametoa wito kwa washiriki kuanza kutoa elimu na hamasa katika maeneo yao ili wananchi waweze kujiandikisha na kunufaika na huduma hiyo.

Kwa upande wao, washiriki wa kikao hicho wamesema kikao kimewapa uelewa mpana kuhusu Bima ya Afya kwa Wote na faida zake. Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Kitendeni, Dkt. Fabian Mtalo, amesema mpango huo utamwezesha mgonjwa kupata matibabu kuanzia ngazi ya zahanati hadi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kupunguza gharama za matibabu na kupata huduma wakati wowote katika vituo vilivyosajiliwa na Serikali.

Aidha, Mjumbe wa Bodi ya Afya ya Wilaya, Paine Lemashon, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha mpango huo, akisema kuwa utawarahisishia wananchi kupata huduma bora, endelevu na za uhakika za afya.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA November 17, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA November 17, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2025 November 05, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • TFFT YATAMBULISHA MRADI WA KUIMARISHA ELIMU YA MSINGI WILAYANI LONGIDO

    January 23, 2026
  • TAKUKURU LONGIDO YATOA ELIMU YA MAADILI KWA WALIMU WAKUU

    January 23, 2026
  • LONGIDO YAWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA UFAULU NA KUBORESHA ELIMU MWAKA 2026

    January 23, 2026
  • DC LONGIDO AKABIDHI MADAWATI 40 SHULE YA MSINGI KITARINI, APONGEZA USHIRIKIANO WA WANANCHI

    January 22, 2026
  • View All

Video

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 29 0KTOBA 2025
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: +255 272 970 793/ 94

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.

  • Situs Toto
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Togel
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • YAMITOTO
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • DORA77
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • KOI200
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Toto Slot
  • DORA77
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto
  • Toto 4D
  • Toto 4D
  • toto
  • Toto 4D
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • toto slot
  • koi200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • Situs Toto
  • KOI200
  • Toto Slot Gacor
  • AERO88 Slot Gacor
  • Slot Gacor
  • Slot Gacor
  • AERO88
  • Situs Toto
  • situs toto
  • slot gacor
  • situs toto
  • yamitoto
  • kudetabet98
  • kudetabet98
  • yamitoto
  • dora77
  • koi200