• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Posted on: June 17th, 2025

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yamefanyika kwa mafanikio makubwa katika viwanja vya Shule ya Msingi Namanga wilayani Longido, yakihudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo, wazazi na wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Katibu Tawala wa Wilaya ya Longido, Bi. Rahma Kondo, aliwapongeza wadau wote wanaojihusisha na ustawi wa watoto kwa kushiriki kikamilifu katika maandalizi na utekelezaji wa maadhimisho hayo muhimu.“Napenda kutoa shukrani za dhati kwa wadau wote wanaoshughulika na masuala ya watoto kwa moyo wa kujitolea, pamoja na kushiriki kikamilifu katika maadhimisho haya.

 

Siku ya Mtoto wa Afrika ni kumbukumbu ya kipekee inayotukumbusha sisi wazazi na walezi juu ya wajibu wetu wa kuhakikisha watoto wanalelewa katika mazingira salama na yenye staha,” alisema Bi. Rahma.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Rajab Mmbunda alieleza kuwa maadhimisho haya ni jukwaa muhimu la kuwakumbusha wananchi kuhusu haki za msingi za watoto, ikiwa ni pamoja na haki ya kupata elimu, afya, ulinzi, na malezi bora.

Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ilikuwa: “Haki ya Mtoto: Tulipotoka, Tulipo na Tuendako,”ikilenga kutathmini hatua zilizopigwa katika kulinda haki za watoto, changamoto zilizopo na mikakati ya kuimarisha ustawi wa watoto barani Afrika.

Mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali yalijitokeza kushiriki na kutoa mchango wao mkubwa katika tukio hilo. Miongoni mwa mashirika hayo ni ACE Africa, CORDS Tembo, Compassion International, na MPDI, ambayo yameendelea kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya mtoto katika wilaya ya Longido kupitia miradi mbalimbali ya elimu, afya, lishe na ulinzi wa mtoto.Maadhimisho hayo yalipambwa na nyimbo,maigizo ngonjera kutoka kwa watoto na wadau mbalimbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • LONGIDO YAAGA MADIWANI WAKE KWA HESHIMA, YASIFIA UONGOZI WAO WA HEKIMA NA BUSARA

    June 20, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    June 17, 2025
  • LONGIDO YATOA VIPAJI KUUNDA TIMU YA MKOA KWENYE MASHINDANO YA UMISSETA

    June 06, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAPELEKA TIMU YA UMITASHUMTA KATIKA MASHINDANO YA MKOA ARUSHA 2025

    May 28, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM