NA MWANDISHI WETU, LONGIDO
Wilaya ya Longido mkoani Arusha mnamo Februari 2, 2026, imeadhimisha Siku ya Sheria katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Longido, ikiwa na lengo la kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria, haki zao na wajibu wao katika jamii.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Longido, Mheshimiwa Eliarusia Ruben Nassary, amesema Mahakama ni taasisi huru inayotekeleza majukumu yake bila kuingiliwa.
“Mahakama ina wajibu wa kuhakikisha kila mwananchi anapata haki kwa wakati na kwa usawa. Kuheshimu sheria ni msingi wa amani na maendeleo,” amesema Mh. Nassary.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salum Kalli, ameipongeza Mahakama kwa mchango wake katika kudumisha amani na utulivu wilayani humo.
“Ushirikiano kati ya Mahakama, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi umechangia kupunguza migogoro na makosa ya jinai wilayani Longido,” amesema Mh. Kalli.
Mhe Kalli amewahimiza wananchi kuendelea kufuata sheria, kutoa taarifa za matukio ya kihalifu na kutatua migogoro kwa njia za kisheria.
Siku ya Sheria huadhimishwa kila mwaka nchini kwa lengo la kuimarisha utawala wa sheria na kuhakikisha haki inapatikana kwa wote.
Arusha- Namanga Road, Longido Town
Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha
Telephone: +255 272 970 793/ 94
Mobile: 0756395889
Email: ded@longidodc.go.tz
Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.