• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA WAZEE KWA SHANGWE NA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA

Posted on: September 26th, 2025

Na Happiness Nselu

Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha leo Septemba 26, 2025 imeadhimisha Siku ya Wazee Duniani kwa kaulimbiu: “Wazee Kushiriki Katika Uchaguzi kwa Ustawi wa Jamii Yetu.” Maadhimisho hayo yamefanyika katika Ukumbi wa J.K. Nyerere, yakihudhuriwa na mamia ya wazee kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya na mkoa mzima.

Shughuli zilizofanyika katika maadhimisho haya ni nyingi na zenye manufaa, ikiwemo:

  • Upimaji wa Afya: vipimo vya shinikizo la damu, sukari, macho na hali ya lishe

  • Ugawaji wa miwani bure kwa wazee waliobainika kuhitaji

  • Burudani 

  • Chakula na vinywaji vya pamoja ambavyo vilikamilisha furaha ya siku hiyo


Kauli za Viongozi

Akizungumza wakati wa maadhimisho, Katibu Tawala Wilaya ya Longido, Bi. Rahma Kondo, alisema Serikali imedhamiria kutoa huduma bora na mikakati madhubuti ya kusaidia wazee, ikiwemo huduma za matibabu na kutatua changamoto za kijamii zinazowakabili.

“Wazee ni hazina ya taifa letu. Ni jukumu letu kama jamii kuendelea kuwatunza, kuwasikiliza na kuwatumia hekima yao katika maendeleo ya kijamii na kitaifa,” alisema Bi. Kondo.

Bi. Kondo pia aliwataka wazee kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, akisisitiza kuwa sauti zao zina mchango mkubwa katika kuimarisha ustawi wa taifa na maendeleo ya jamii.

Kwa upande wao, Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa Bw. Denis Mgiye, Afisa Ustawi Wilaya Bw.A bdalah Nyange pamoja na Mwenyekiti wa Wazee walitoa salamu kwa wazee, wakisisitiza mshikamano, heshima, na umuhimu wa kizazi kipya kujifunza kutoka kwa hekima na uzoefu wa wazee.

Furaha ya Wazee

Wazee waliohudhuria walifurahia sana siku hiyo, wakicheza, kuimba, kula na kunywa pamoja na viongozi na wananchi. Wengi walieleza kuwa maadhimisho hayo yamewapa matumaini mapya na kuthibitisha kuwa bado wanathaminiwa na taifa.

Historia Fupi ya Siku ya Wazee

Siku ya Wazee Duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo Oktoba 1 tangu ilipoanzishwa na Umoja wa Mataifa mwaka 1990. Lengo kuu ni kutambua mchango wa wazee katika jamii, kuhakikisha haki zao zinalindwa, na kuhamasisha ustawi wao wa kijamii, kiuchumi na kiafya. Tanzania imekuwa ikishiriki maadhimisho haya kila mwaka kwa kutoa huduma za kijamii na kiafya kwa wazee, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuthamini na kuenzi wazee.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA WAZEE KWA SHANGWE NA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA

    September 26, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    September 20, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    September 20, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    September 20, 2025
  • View All

Video

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII WILAYA YA LONGIDO
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.