• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

Posted on: July 11th, 2025

Na Happiness Nselu 

Halmashauri ya Wilaya ya Longido imepokea tuzo ya pongezi kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI baada ya kufanikisha lengo la ufaulu lililowekwa kwenye Key Performance Indicator (KPI) katika Upimaji wa Kitaifa wa Kidato cha Pili kwa mwaka 2024.

Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwa mara ya kwanza wakati wa mkutano wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri uliofanyika katika Manispaa ya Iringa, ambapo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI – Elimu, Ndg. Atupele W. Mwambene, aliipongeza Halmashauri ya Longido kwa mafanikio hayo ya kitaaluma.

Akizungumza katika kikao hicho, Ndg. Mwambene alisema kuwa Longido imeonyesha mfano wa kuigwa katika kusimamia taaluma, kuwajengea walimu mazingira bora ya kufundisha na kushirikisha jamii katika maendeleo ya elimu.

“Tumeona matokeo ya juhudi zenu. Longido ni miongoni mwa halmashauri zilizofikia viwango vya ufaulu tulivyovitarajia. Hili ni jambo la kujivunia,” alisema.

Mara baada ya kuwasili Longido, tuzo hiyo imekabidhiwa rasmi leo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Nassoro Shemzigwa, ambaye alipokea kwa niaba ya timu nzima ya elimu ya halmashauri hiyo.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Shemzigwa ameishukuru TAMISEMI kwa kutambua juhudi za halmashauri yake, na kusema kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya mshikamano, nidhamu ya kazi na usimamizi mzuri wa walimu pamoja na viongozi wa elimu katika ngazi zote.

“Tuzo hii ni motisha kubwa kwetu. Itaendelea kutusukuma kufanya vizuri zaidi, si tu kwa Kidato cha Pili, bali katika nyanja zote za elimu,” alisema Shemzigwa.

Kwa mujibu wa takwimu kutoka TAMISEMI, Longido imepanda kwa kasi katika viwango vya ufaulu ikilinganishwa na miaka ya nyuma, jambo linaloashiria ufanisi wa mikakati ya kuinua kiwango cha elimu vijijini.

Hii ni mara ya kwanza kwa Halmashauri ya Wilaya ya Longido kutunukiwa tuzo ya aina hiyo, hatua inayoweka historia mpya na kuongeza hamasa kwa wadau wa elimu wilayani humo.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • WAZIRI WA MIFUGO AZINDUA CHANJO YA MIFUGO ,AWATAKA WAFUGAJI KUFUGA KISASA

    July 02, 2025
  • LONGIDO YAAGA MADIWANI WAKE KWA HESHIMA, YASIFIA UONGOZI WAO WA HEKIMA NA BUSARA

    June 20, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM