• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MBIO ZA MWENGE WA UHURU LONGIDO ZAZINDUA NA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI

Posted on: June 8th, 2019

Maendeleo ni namna ya kutoka hatua moja iliyo ya chini kwenda hatua nyingine ya juu kimafanikio. Ujenzi wa Miradi ya maendeleo ni swala mtambuka kwa maana halina mwisho na sababu kubwa ya kupelekea ujenzi wa Miradi ya maendeleo kutokuwa na mwisho ni kutokana na ongezeko la uhitaji wa huduma za kijamii, kisiasa na kiuchumi kila kuhitwapo leo.

Mbio za mwenge wa Uhuru ndio dhana kubwa ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania iliyojidhatiti katika uzinduzi ,ukaguzi na utembeleaji wa Miradi ya Maendeleo kama Viwanda, Barabara, Shule, Maji n.k. katika kila mwaka na kupitia Halmashauri mbalimbali.

Halmashauri ya Wilaya ya Longido mkoani Arusha ni miongoni mwa Halmashauri changa toka kuanzishwa kwake mwaka 2007 lakini imepiga hatua kubwa hasa katika ukusanyaji kodi, utekelezaji wa Miradi ya maendeleo kama miundombinu ya Maji, Barabara, umeme, ujenzi wa Vituo vya Afya kama Hospitali ya Wilaya, Soko la Madini, Kiwanda cha kusindika Nyama n.k.

Tarehe 07.06.2019 ni siku ya kipekee katika mwaka 2019 katika Wilaya ya Longido kwa kumbukumbu ya mbio za Mwenge wa Uhuru uliopita katika maeneo mbalimbali kwa uzinduzi, ukaguzi na utembeleaji wa Miradi mbalimbali iliyokwisha tekelezwa na  inayoendelea kutekelezwa kwa kuweka Mawe ya Msingi, kuangalia namna utekelezaji unavyoendelea/kuendeshwa pamoja na kutoa ushauri na mapendekezo katika sehemu zinazohitaji maboresho.

Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Longido umetembea Kilomita 202.5, umepita katika Trafa mbili kati ya nne zilizopo ambazo ni Kitumbeine na Longido pia umekimbizwa Kata sita kati ya 18 na ulipita katiuka vijiji 10 kati ya 49 vya Wilaya ya Longido.s

Zoezi zima la uzinduzi, ukaguzi na utembeleaji wa Miradi limeanzia mnamo saa 4:00 asubuhi mara baada ya shughuli  ya kuupokea Mwenge wa Uhuru lililoanza saa 2:30 asubuhi  katika viwanja vya kata ya Gelai Merugoi vinavyo zitenganisha Wilaya mbili yaani Longido na Ngorongoro chini ya kiongozi mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2019 Mzee Mkongea Ali.  Katika uzinduzi wa Miradi hiyo amegusia Sekta za Elimu, Maji, Uhifadhi wa Mazingira, Viwanda na uwekezaji wananchi kiuchumi.

Jumla ya Miradi iliyokaguliwa, kuwekwa mawe ya msingi na kutembelewa jumla ni saba ambapo mitano ilikaguliwa/ kutembelewa na miwili iliwekwa mawe ya msingi. Miradi yote hii ilikuwa na thamani shilingi billion ishirini na saba, million miasaba kumi na nne , sabini na tisa elfu,mia nane kumi na saba na senti ishirini (Tsh. 27,714,079,817.20).

Mzee Mkonge Ali mkuu wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa 2019 amekagua/kutembelea Mradi uliokamilika wa madarasa matatu pamoja na madawati sitini (60) katika shule ya Msingi Ketumbeine wenye thamani ya Tsh. 53,450,000/= na kuridhika na ujenzi wa Mradi huo. Mradi mwingine ambao uliwekwa jiwe la Msingi na ujenzi wa Bweni la Wasichana wa Tanzania Education and Micro-Business Opportunity (TEMBO  Trust) wanye thamni ya Tsh. 207,331,673.20 na kuridhishwa na utekelezaji huo.

Lakini pia Mkongea Ali Mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa ametembelea na kukagua utekelezaji wa Mradi mkubwa wa Tanki la Maji ambao umefikia 98% kwa thani ya Tsh. 15,793,939,144 na tayali Tsh. 10,195,410,690.78 zimekwisharipwa kwa mkandarasi, ameridhishwa na mwendelezo huo. Hatahivyo ameweka jiwe la Msingi na kuzindua Mradi wa Mali Hai Club na Uhifadhi wa Mazingira katika shule ya Sekondari  Longido ambapo ameridhishwa jinsi ambavyo Wilaya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, Mashirika binafsi pamoja na Longido Sekondari kuhakikisha wanatunza Mazingira hasa ndani ya Longido yanayoonekana kuwa na ukame.

Vilevila Ndug. Mkongea Ali alizindua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kiwanda kikubwa cha usindikaji nyama  cha Eliya Food Overseas Ltd ambacho kinalenga kutekeleza Irani ya Chama Cha Mapinduzi ya Serikali ya awamu ya tano kuwa ni Serikali ya Viwanda  ambacho ujenzi wake umefikia 70%  kinatarajia kukamilika na kuanza uzalishaji Oktoba 2019. Kiwanda hicho hadi kukamilika kwake kinatarajiwa kutumia jumla ya Tsh. 11,600,000,000.00

  

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM