• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

MIRADI YA MAJI KUKAGULIWA NCHI NZIMA

Posted on: April 11th, 2017

SERIKALI inafanya mapitio na kufanya uchunguzi wa miradi yote ya maji nchini ili kubaini inayofanya kazi na isiyofanya kazi.

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isack Kamwelwe alitoa uhakika huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mufindi Kusini, Menrad Kigola (CCM) aliyetaka kujua Serikali inafanyika nini kuboresha miradi ya maji iliyoanzishwa, lakini haifanyi kazi.

Alisema serikali inapitia miradi hiyo ikiwamo ya maji iliyojengwa Mufindi Kusini ambako matangi 11 yalijengwa, lakini hayana maji.

Naibu Waziri alisema mara uchunguzi huo utakapokamilika, mkakati wa Serikali utakuwa kuboresha miundombinu ya maji ikiwamo kusafisha matangi na visima vilivyochimbwa ambavyo havina maji ili kuhakikisha vinafanya kazi.

Akijibu swali la msingi la mbunge huyo aliyetaka kujua serikali itamaliza lini ujenzi wa mradi wa Maji Sawala, Mtwango, Lufuna na Kibao, Kamwelwe alisema mradi huo ulianza kutekelezwa Juni mosi, 2015 na ulitarajiwa kukamilika Juni mosi, mwaka jana.

Alisema utekelezaji wa mradi huo ulipangwa kufanyika kwa awamu tatu ambazo ni kujenga mahali pa kutega maji na kupeleka maji katika kijiji cha Sawala.

Awamu ya kwanza ya utekelezaji imefanyika katika kijiji cha Sawala kwa gharama ya Sh milioni 644.21 na hadi sasa Sh milioni 261.64 zimetumika katika mradi huo.

Kazi zilizotekelezwa hadi sasa ni pamoja na ujenzi wa mahali pa kuchukua maji, visima, boma za nyumbani na ulazaji wa bomba kuu, ujenzi wa tangi mita za ujazo 200 na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 16 na ehemu ya mabomba ya usambazaji kilometa 3.4 kwa wastani wa kazi umefanyika kwa asilimia 50 kwa kijiji cha Sawala tu.

Mradi huo haukukamilika kwa wakati kutokana na mkandarasi kushindwa kukamilisha kazi kwa mujibu wa mkataba.

Novemba mwaka huu, halmashauri ya wilaya ya Mufindi ilivunja mkataba na mkandarasi huyo, na kuamua kutangaza upya Februari 7, mwaka huu ili kumpata mpya.

Mkandarasi anatarajiwa kupatikana Juni mwaka huu, na kazi itakamilika katika mwaka huu wa fedha.


Chanzo Habari Leo. By Joseph P Mkumbwa

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.