• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA ARUSHA ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA HOSPITALI KUBWA LONGIDO

Posted on: June 9th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Longido Mkuu wa Mkoa wa Arusha Chini usimamizi wa umakini wa hali ya kuridhisha wa Mkurugenzi Mtendaji  Ndug. Jumaa Muhina  imepewa pongezi kwa uendelezaji mzuri wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya hiyo ambao kwa sasa umefikia hatua ya kupaua/ kuwezeka kwa baadhi ya majengo.

Bw. Mrisho Mashaka Gambo mkuu wa Mkoa wa Arusha ametoa pongezi hizo mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea na kukagua mwendelezo wa utekelezaji wa Mradi huo unaotekelezwa ndani ya Wilaya ya Longido na kujionea jinsi namna ujenzi unavyoenda kwa kasi.

Bw. Gambo amesema kuwa Mkoa wa Arusha umepata fursa ya kipekee ya kujengewa vituo vya Afya na Serikali ya awamu ya tano katika maeneo mbalimbali na kuwataka Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na wahusika wa utekelezaji wa Mradi huo mkubwa Longido kufanya kazi usiku na mchana ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Mgufuli kwa kauli mbiu ya ‘HAPA KAZI TU!’.

Aidha Gambo amesema kuwa Mradi wa utekelezaji ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ulitarajiwa kumalizika mwezi Mei 2019 lakini kutokana na ukubwa wa Mradi pomoja na vifaa kutoka mbali huku vikitumika kona nyingi za Tanzania ambazo Hospitali/Vituo vya Afya vinajengwa upelekea Mradi huo kuongezewa muda. Vilevile Bw. Gambo amewasihi kuhakikisha kufika mwezi Juni 30, 2019 Mradi huo uwe umekamilika.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mhe. Frank James Mwaisumbe amesema kuwa utekelezaji wa Mradi huo mkubwa ndani ya Longido pindi utakapokamilika utawaondolea hadha wakazi wa Longido ya kusafili umbali mrefu kwenda Arusha ama KCMC  kutafuta matibabu, Wasafili wanaotoka ama kwenda nchi jirani Kenya kwa maana Mradi upo karibu na barabara kwahiyo utatoa huduma kwa haraka, magonjwa ya akina mama na watoto yatatatuliwa, upasuaji pamona na huduma nyingine za kiafya ambazo zimekuwa zikiwasumbua wanalongido zitapatiwa majibu.

Hata hivyo Mhe. Mwaisumbe amefafanua kuwa Mradi huo unajumla ya majengo saba (7) yanayo jumuisha Wodi ya wazazi, jingo la upasuaji, Wodi ya kulaza wagonjwa, Wodi ya akina mama na watoto, Chumba cha dharura na maeneo mengine kwa ajili ya kutoa huduma za kiafya.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Wilaya kwa kushirikiana na Mkurugenzi wakuu wa Idara, Engineer kutoka Arusha wamekwisha ridhia toka awali kufanya kazi usiku na mchana ili kumaliza kwa wakati.

Naye mkurugenzi Jumaa Mhina amesema ujenzi umefika hapa mahala pazuri kwa ushirikiano mkubwa wa Serikali pamoja na Wanalongido kwa ujumla kwa kujitoa usiku na mchana kuiunga mkono serikali ya Tanzania.

Pia ameendelea kusema kuwa Serikali imetupa kipaumbele cha kutujengea Hospitali kubwa Ya Wilaya hivyo na wao kama Halmashauri wanajibbika kwa kutekeleza Mradi huo kwa kiwango stahiki na kwa muda muafaka.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM