• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

MKUU WA MKOA ARUSHA ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA HOSPITALI KUBWA LONGIDO

Posted on: June 9th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Longido Mkuu wa Mkoa wa Arusha Chini usimamizi wa umakini wa hali ya kuridhisha wa Mkurugenzi Mtendaji  Ndug. Jumaa Muhina  imepewa pongezi kwa uendelezaji mzuri wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya hiyo ambao kwa sasa umefikia hatua ya kupaua/ kuwezeka kwa baadhi ya majengo.

Bw. Mrisho Mashaka Gambo mkuu wa Mkoa wa Arusha ametoa pongezi hizo mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea na kukagua mwendelezo wa utekelezaji wa Mradi huo unaotekelezwa ndani ya Wilaya ya Longido na kujionea jinsi namna ujenzi unavyoenda kwa kasi.

Bw. Gambo amesema kuwa Mkoa wa Arusha umepata fursa ya kipekee ya kujengewa vituo vya Afya na Serikali ya awamu ya tano katika maeneo mbalimbali na kuwataka Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na wahusika wa utekelezaji wa Mradi huo mkubwa Longido kufanya kazi usiku na mchana ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Mgufuli kwa kauli mbiu ya ‘HAPA KAZI TU!’.

Aidha Gambo amesema kuwa Mradi wa utekelezaji ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ulitarajiwa kumalizika mwezi Mei 2019 lakini kutokana na ukubwa wa Mradi pomoja na vifaa kutoka mbali huku vikitumika kona nyingi za Tanzania ambazo Hospitali/Vituo vya Afya vinajengwa upelekea Mradi huo kuongezewa muda. Vilevile Bw. Gambo amewasihi kuhakikisha kufika mwezi Juni 30, 2019 Mradi huo uwe umekamilika.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mhe. Frank James Mwaisumbe amesema kuwa utekelezaji wa Mradi huo mkubwa ndani ya Longido pindi utakapokamilika utawaondolea hadha wakazi wa Longido ya kusafili umbali mrefu kwenda Arusha ama KCMC  kutafuta matibabu, Wasafili wanaotoka ama kwenda nchi jirani Kenya kwa maana Mradi upo karibu na barabara kwahiyo utatoa huduma kwa haraka, magonjwa ya akina mama na watoto yatatatuliwa, upasuaji pamona na huduma nyingine za kiafya ambazo zimekuwa zikiwasumbua wanalongido zitapatiwa majibu.

Hata hivyo Mhe. Mwaisumbe amefafanua kuwa Mradi huo unajumla ya majengo saba (7) yanayo jumuisha Wodi ya wazazi, jingo la upasuaji, Wodi ya kulaza wagonjwa, Wodi ya akina mama na watoto, Chumba cha dharura na maeneo mengine kwa ajili ya kutoa huduma za kiafya.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Wilaya kwa kushirikiana na Mkurugenzi wakuu wa Idara, Engineer kutoka Arusha wamekwisha ridhia toka awali kufanya kazi usiku na mchana ili kumaliza kwa wakati.

Naye mkurugenzi Jumaa Mhina amesema ujenzi umefika hapa mahala pazuri kwa ushirikiano mkubwa wa Serikali pamoja na Wanalongido kwa ujumla kwa kujitoa usiku na mchana kuiunga mkono serikali ya Tanzania.

Pia ameendelea kusema kuwa Serikali imetupa kipaumbele cha kutujengea Hospitali kubwa Ya Wilaya hivyo na wao kama Halmashauri wanajibbika kwa kutekeleza Mradi huo kwa kiwango stahiki na kwa muda muafaka.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.