• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

TUTAENDELEA KUWA WAJINGA MPAKA LINI, MHE. GAMBO

Posted on: June 20th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo ameiomba Wizara ya Kilimo na Mifugo kuzitafutia ufumbuzi changamoto walizozitoa wafanyabiashara wa Soko la kuuza na kununua Mifugo la Eworendeke lililopo Namanga Wilayani Longido mkoani Arusha.

Maombi hayo ameyatoa leo jioni juni 20, 2019 wakati akilasimisha/kufungua  Soko hilo ambalo linalenga kutatua changamoto za wafanyabiashara wa Mifugo, kukuza uchumi pamoja na kuitangaza nchi kwa kutoa huduma ya mifugo na nyama kila siku.

Mhe. Gambo ambaye alikuwa mgeni rasmi amesema kuwa malengo ya kulasimisha soko hilo ni kuondoa utoroshwaji wa mifugo bila kufuata utaratibu, Kupunguza kodi zisizo za lazma kwani wafugaji wanafanya kazi kubwa ya kuchunga ng’ombe na kuwatunza, kutengwa kwa mapato ya serikali na haki ya mfugaji ili maji barabara,elimu bure na miundombinu nyingne ziweze kujengwa.

 Aidha amesema kuwa baada ya kufungua soko hilo mkoa utaimarisha ulinzi wa mipaka mara dufu na kuchunguza kwa umakini kule wafanyabiashara wanakouza ng’ombe kama wameuzwa kwa njia halali ili kuhakikisha muuzaji na mnunuzi wote wanapata haki zao na pale itakapobainika mifugo inatoroshwa wahusika watawajibishwa.

Vilevile amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Longido kuandaa kikao cha kuwakutanisha wafanyabiashara wa pande zote mbili yaani Tanzania na Kenya ili kuondoa utofauti na kama akishindwa amtaarifu mkuu wa Mkoa na mkuu wa mkoa akishindwa bazi Wizara itapatiwa taarifa kikubwa mpaka mwafaka upatikane.

Hata hivyo amezungumza kwa ukali kuwa Tanzania itaendelea kuwa ujinga mpa lini kwa kuuza mbuzi Kenya na Kenya kusifika kwa umaarufu wa kufuga kuliko Tanzania “ tutaendelea kuwa wajinga mpa lini tunawauzia mifugo yetu kwa gharama nafuu na mkifika huko mnatamba kuwa mifugo hiyo ni ya kwenu na kupata umaarufu nje ya nchi nasikia huko India tutashindwana kama ni hivyo” Mhe. Gambo

Kwa upande wake Katibu mkuu Wizara ya kilimo na uvuvi Mhe.Elisante Ole Gabriel aliye mwakilisha Waziri wa Kilimo na Mifugo amesema kuwa swala la ufunguzi wa soko hilo la kimataifa litaleta neema katika nchi kwani toka 2001 mapendekezo yalikuwepo na mwaka agosti 31, 2019 mradi huo ulipitishwa kuwa mnada wa mpakani.

Mhe. Ole amesema kuwa jitihada zilizofanywa na Ofisi ya Waziri mkuu, Mkoa, Wilaya pamoja na wadau wengine vimekuwa chachu kubwa katika ujenzi mpaka kufikia hatua za ufunguzi. Pia amesema kuwa Waziri amemwagiza kuwa wafanyabiashara wasidhubutu kutorosha mifugo.

Ameendelea kusema kuwa Wizara inategemea wananchi wafuge kwa tija, wasijivunie idadi ya ng’ombe bali wajivunie uzito wa ng’ome, na mnada usiwe patio la mifugo bali wapime ng’ombe wauze kwa kilo.

Mhe. Frank Mwaisumbe Mkuu wa Wilaya Longido amesema kuwa ataandaa kikao cha wafanyabiashara wa mifugo na mmiliki wa kiwanda kikubwa kinachojengwa ili kujua nini atahitaji kwao na wao wamweleze nini wanahitaji kwake. Vilevile ametaja siku za juma tatu na juma nne ni kuuza mifugo tu, juma tano licha ya kuuza mifugo lakini kutakuwepo mnada yaani kuchoma nyama, kuchinja n.k, alihamisi – jumamosi ni kuuza mifugo tu na juma pili kutakuwepo na michezo mbalimbali kwaajili ya kutangaza utalii na huduma zinazopatikana sokoni hapo.

Ufunguzi huo umehudhuriwa Mkuu wa Wilaya wa Monduli Mhe. Idda Kimanta, mwakilishi wa DC upande wa kenya Steven Komara ,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido Mhe. Sambore Molloimet,Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Longido Ndg. Jumaa Mhina, wafanyabiashara, wakuu wa usalama pamoja na wananchi  

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.