• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YATEKELEZA KWA ASILIMIA MIA AGIZO LA MH.RAISI KWA KUWAPATIA VIKUNDI 11 MKOPO USIO NA RIBA.

Posted on: October 31st, 2018

 Halmashauri ya wilaya ya longido Leo tarehe 31/10/2017  imetoa mkopo usio na riba wa fedha za kitanzania sh.42,630,000/- kwa vikundi  kumi na moja  vya kina mama, vijana na walemavu

Kaimu Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Wilaya Nd. Raymond Mushi wakati wa sherehe za makabidhiano hayo amesema vikundi hivyo   ni vya Wanawake,Vijana na Walemavu ambavyo vinajishughulisha na ufugaji, ushonaji shanga na urembo wa kimasai,vikoba na biashara ndogondo.

Mushi amevitaja vikundi hivyo ni Tenebo,Nasaruni parmanja,,Osotwa,Yeyowomen group,Tobiko,Naramatisho,Mshikamano,Amani na Upendo,Upendo groupA2017,Nasaro na Nyangulo armanie.

 Pia Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido  Nd. Jumaa Mhina wakati wa makabidhiano hayo amesema pesa hizo zinazotolewa za mikopo  ni  za mapato ya ndani  ya Halmashauri ya Wilaya ya Longido na mkopo unatolewa  bila riba yoyote kwa vikundi vyote ikiwa ni kutekeleza agizo la  Mh Rais wa awamu ya tano  Mh.John Pombe Magufuli la kutoa asilimia 10%  ya mapato  ya ndani kwa wanawake asilimia 4%,vijana asilimia 4%, walemavu asilimia 2% na mkopo huo usio na riba kwa robo hii ya kwanza ya mwaka wa fedha 2018/2019 umetolewa kwa asilimia 100% .

Akikabidhi mikopo hiyo mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Longido ndg.Frank Mwaisumbe ,amewaasa wanavikundi kuwa pesa zinazotolewa Leo ni kwa ajili ya kukuza uchumi na kuongeza kipato cha wanavikundi na si kwa matumizi mengine lakini pia amewasisitiza kurudisha mikopo hiyo ili isaidie na  wahitaji wengine.

Nae Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Ndg. Loth Sanare ameupongeza uongozi wa wilaya kwa kazi nzuri ya kufanya hitaji la kisheria la kutoa asilimia mia moja ya mkopo kwa vikundi mbalimbali lakini pia kuwa mstari wa mbele katika kushughulikia shida za wananchi kama anavyotutaka Mh.Rais wetu wa awamu ya tano  kuwa tushughulike na shida za wananchi.

Mwenyekiti Sanare pia ameviasa vikundi vyote kurudisha mikopo hiyo kwa wakati pindi muda utakapofika ili vikundi vingine vipate mikopo hiyo.

 Vile vile vikundi vilivyopata mikopo wametoa shukrani zao za dhati kwa Halmashauri ya Longido na kuahidi kutumia mikopo hiyo kama ilivyokusudiwa.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM