• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA RASMI KAZINI WAAPISHWA LEO

Posted on: December 2nd, 2024

Na Happiness  Nselu 

Longido, Arusha - Viongozi wapya wa serikali za mitaa katika Wilaya ya Longido wameapishwa rasmi leo katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, watendaji wa halmashauri, na wananchi waliokuja kushuhudia tukio hilo muhimu.

Hakimu mfawidhi wa Wilaya ya Longido  Mh.Eliarusia R.Nassary aliwaongoza viongozi hao katika kiapo cha uadilifu na uwajibikaji. Akizungumza baada ya kuwaapisha,Bw. Joseph Logolie aliwahimiza viongozi hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa weledi, uwazi, na kushirikiana na wananchi katika kusukuma mbele maendeleo ya jamii zao.


“Uongozi ni dhamana, na jukumu lenu kubwa ni kuhakikisha mnatoa huduma bora kwa wananchi wenu. Msikilize matatizo yao, tafuteni suluhisho kwa kushirikiana, na hakikisheni mnazingatia sheria na kanuni za utumishi wa umma,” alisisitiza Bw Logolie.


Viongozi walioapishwa ni pamoja na wenyeviti wa vijiji, wenyeviti wa vitongoji, na wajumbe wa halmashauri kundi la wanawake pamoja na wajumbe kundi mchanganyiko mbalimbali  Pia walikabidhiwa nyaraka muhimu zinazowaongoza kutekeleza majukumu yao, ikiwa ni pamoja na mwongozo wa usimamizi wa miradi ya maendeleo na utawala bora.


Akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake, Mwenyekiti mpya wa Kijiji cha Orkojoolengush Bw.Lekshon Kaika Mollel  aliahidi kuwajibika kwa moyo wa dhati na kuhakikisha wanashirikiana na wananchi kuboresha maisha ya jamii.


Kufuatia kuapishwa kwao, viongozi hawa wanatarajiwa kuanza mara moja kusimamia shughuli za maendeleo katika maeneo yao, kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya kuhakikisha Longido inaendelea kupiga hatua katika nyanja za kijamii na kiuchumi.


“Kwa pamoja tutaweza, na Longido itaendelea kuwa mfano wa kuigwa katika uongozi na maendeleo,” alihitimisha Bw. Joseph



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 08, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA ( LINARUDIWA ) October 10, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA October 19, 2024
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA LONGIDO AWATAKIA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA KILA LAHERI KWENYE MITIHANI YAO

    September 09, 2025
  • HUDUMA ZA UPASUAJI ZAANZA RASMI KITUO CHA AFYA EWORENDEKE - LONGIDO

    September 06, 2025
  • HUDUMA ZA UPASUAJI ZAANZA RASMI KITUO CHA AFYA EWORENDEKE - LONGIDO

    September 06, 2025
  • RC ARUSHA ATOA WITO WA AMANI NA UTULIVU LONGIDO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    September 04, 2025
  • View All

Video

PWC YATOA MSAADA KWA MASHIRIKA MADOGO LONGIDO KUKABILI MABADILIKO YA TABIA NCHI
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.