NA MWANDISHI WETU
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Longido imewakabidhi zawadi Walimu Wakuu watatu kwa kutambua usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo katika shule zao.
Walimu waliotunukiwa ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Sinya, Mwalimu Andrew Tekwi, Mkuu wa Shule ya Sekondari Longido, Mwalimu Justin Swai, na Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Sinya, Mwalimu Deodatus Utouh.
Zawadi hizo zilikabidhiwa Januari 30, 2026 na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Longido, Mhe. Papaa Nakuta Mollel, wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido (JK Nyerere).
Akizungumza wakati wa makabidhiano, Mhe. Mollel aliwasifu walimu hao kwa uzalendo na ufanisi katika kusimamia miradi hadi kukamilika kwa wakati.
Aliwataka walimu wengine kujifunza kutoka kwao kwa kutembelea shule husika ili kuongeza ujuzi wa usimamizi wa miradi ya maendeleo.
Arusha- Namanga Road, Longido Town
Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha
Telephone: +255 272 970 793/ 94
Mobile: 0756395889
Email: ded@longidodc.go.tz
Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.