• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

WANAFUNZI 219 WAHITIMU KIDATO CHA NNE SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR

Posted on: October 6th, 2025

NA ABRAHAM NTAMBARA, LONGIDO

Jumla ya wanafunzi 219 wamehitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Engarenaibor iliyopo Kata ya Engarenaibor Wilaya ya Longido mkoani Arusha.

Wahitimu hao ni sehemu ya waafunzi 327 walioanza kidato cha kwanza mwaka 2022 ambapo imeelezwa kuwa baadhi yao hawakuhitimu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo za ujauzito, utoro na kuhama shule.

Akizungumza katika mahafali ya 16 yaliyofanyika Oktoba 3, 2025 shuleni hapo, Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanabonde Investment Antony Mngodo alitoa wito kwa wanafunzi hao kufuta daraja la sifuri (Division 0) na kuhakikisha wanapata daraja la kwanza (Division I) na daraja la pili (Division II) katika mtihani wao wa NECTA unaotarajia kuanza Oktoba 13 mwaka huu.

Mngodo aliupongeza uongozi na waalimu wa shule hiyo kwa kuwaandaa vyema wanafunzi hao ili kuhakikisha wanafanya vizuri katika mtihani wao.

"Nawapongeza wanafunzi mliofikia hatua hii leo na Mungu awatunze hadi kwenye mtihani wenu. Nyie mmechaguliwa kufanya mtihani, hivyo mhakikishe mnafanya vizuri," alisema Mngodo na kuongeza,

"Walimu nawapongeza pia kwa kazi nzuri mliyoifanya na kuhakikisha mnafuta daraja sifuri kwa wanafunzi hawa, kufuta hizi sifuri ni mafanikio makubwa kwenu walimu. Tunawapongeza walimu kwa kazi hii kwani sio kazi nyepesi,".

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Longido Mwl. Gilbert Sombe alisema kuwa kutokana na maandalizi yaliyofanyika kwa wanafunzi hao kuelekea mtihani wao wa mwisho, hawategemei mwanafunza yeyote kupata daraja sifuri.

"Katika Shule hii tumepambana kuhakikisha tunaziondoa Division 0 (Daraja Sifuri), kwahiyo hatutegemei kuwa na sifuri," alisema Mwl. Sombe.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwl. Honest Kilewo alisema kuwa idadi ya wanafunzi waliohitimu katika mahafali hayo ya 16 ni 219 na aliwahakikishia wazazi na wananchi kuwa kutokana na maandalizi makubwa waliyowafanyia watafanya vizuri mtihani.

Hata hivyo alitoa wito kwa wazazi kuwa karibu na watoto wao hususan wanapokuwa nyumbani kipindi cha likizo kwani kuwa mbali nao kunachangia kuporomoka kwa maadili ya watoto ambapo ameeleza kuwa kwa kpindi cha Januari hadi Oktoba mwaka huu Shule hiyo imevunja rekodi ya kuwa na wanafunzi 17 waliopata ujauzito.

Kwamba wanafunzi waliopata ujauzito kwa kidato cha kwanza ni watatu (3), kidato cha pili watatu (3), kidato cha tatu 10 na kidato cha nne mmoja (1) na kufanya jumla kuwa wanafunzi 17.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • WANAFUNZI 219 WAHITIMU KIDATO CHA NNE SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR

    October 06, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA WAZEE KWA SHANGWE NA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA

    September 26, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    September 20, 2025
  • LONGIDO YAADHIMISHA SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    September 20, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.