Shirika la RECODA leo, Novemba 21, 2025, limeendesha mafunzo ya kilimo cha bustani ndogondogo za nyumbani kwa wanavikundi kutoka vijiji vya Orbomba, Kimokouwa na Eworendeke, pamoja na taasisi za dini wilayani Longido.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, mwezeshaji Bw. Kaleb Masam alisema kuwa lengo ni kuhakikisha kila kaya inakuwa na uhakika wa mboga za kutosha ili kuongeza lishe pamoja na kujipatia kipato kwa familia na jamii kwa ujumla.
Kwa upande wake, Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Fula Justine, alisema kuwa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka, kwani kilimo cha bustani ni muhimu katika kuzalisha mboga mboga zinazosaidia kuimarisha afya na kuongeza kipato.
Naye Bi. Hadija Rashid, mshiriki na mnufaika wa mafunzo kutoka Eworendeke, amelishukuru Shirika la RECODA kwa kutoa mafunzo hayo ambayo yatasaidia kuongeza lishe na upatikanaji wa mboga katika milo ya nyumbani.
Aidha, Bi. Hellena Laizer, mshiriki kutoka Kimokouwa, alisema kuwa mradi huo ni fursa nzuri ya kuanza kufanya kilimo cha mboga mboga na miche midogo midogo, kisha kuuza ili kuongeza kipato cha familia
Arusha- Namanga Road, Longido Town
Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha
Telephone: +255 272 970 793/ 94
Mobile: 0756395889
Email: ded@longidodc.go.tz
Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.