• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

Posted on: March 21st, 2025

Na Happiness Nselu


*Longido, Machi 21, 2025* - Wataalamu kutoka Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe, wakiongozwa na Mratibu wa Elimu ngazi ya Jamii, Bw. Wasele, leo wamefanya ziara katika shule ya Sekondari Ketumbeine na Engarenaibor, kutoa elimu muhimu kuhusu ugonjwa wa mpox na magonjwa mengine yanayoathiri jamii.


Akizungumza kwa njia ya simu, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Longido, Dkt. Dioniz Methew Majani, alisema kuwa idara yake imejipanga kikamilifu kukabiliana na ugonjwa wa mpox. Alisema kuwa kupitia utoaji wa elimu na mikutano ya jamii, wameweza kuhamasisha wananchi kuhusu hatua za tahadhari na jinsi ya kujikinga dhidi ya maambukizi.


“Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe imejizatiti kutoa taarifa sahihi kwa wananchi ili kupunguza maambukizi ya ugonjwa huu. Tunasisitiza umakini na ushirikiano kutoka kwa kila mmoja wetu katika kudhibiti mambukizi. Huduma za afya zipo, na tunahakikisha kwamba jamii inapata elimu ya kutosha kuhusu magonjwa haya,” alisema Dkt. Majani.


Bw. Wasele aliongeza kuwa, mbali na elimu kuhusu mpox, wamejizatiti pia kutoa huduma za lishe kwa wananchi. Lishe bora, alisema, ni muhimu katika kujenga kinga ya mwili dhidi ya magonjwa. Aidha, alisisitiza kuwa elimu hii ni sehemu ya juhudi kubwa za serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na lishe. Alisema kuwa, "Kwa kushirikiana, tunaweza kupunguza madhara ya magonjwa haya na kuhakikisha afya ya jamii inaboreshwa."


Ziara hii inatolewa kama sehemu ya mkakati wa serikali kuongeza ufahamu kuhusu magonjwa yanayoathiri jamii na kupunguza madhara yake kwa kupitia elimu, ushirikiano na huduma za afya bora. Idara ya Afya pia inaendelea kufanya kazi kwa karibu na viongozi wa mitaa, mashirika yasiyo ya kiserikali, na jamii kwa ujumla, ili kuhakikisha taarifa sahihi zinawafikia wananchi wote.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.