• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZEE KUTIBIWA BURE LONGIDO

Posted on: March 21st, 2019

Na.  Zaina  Mzee.

Mkuu wa wilaya ya Longido Mh Frank James Mwaisumbe leo tarehe 21/03/2019 katika ofisi ya kijiji cha Longido,amegawa vitambulisho vya matibabu  kwa wazee wenye zaidi ya miaka sitini.Wazee zaidi ya themanini wamepata vitambulisho hivyo ikiwa ni kwa awamu ya kwanza tu.Mh Mwaisumbe amewaambia wazee hao kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha wanapata huduma za afya  bure kwa kutambua mchango wao katika kujenge nchi enzi wakiwa vijana na sasa ni wakati wao kufurahia matunda ya nchi yao. aidha amewataka wazee hao kuhakikisha wanatunza vitambulisho vyao ili waweze kutibiwa na wasipate usumbufu wowote kwenye vituo vya afya.  "wazee ni hazina na palipo na wazee hapaharibiki kitu natumai uwepo wenu kwenye nchi yetu ni baraka kubwa sana hata nasi vijana tunapo waona tunajivunia hivyo sisi kama serikali tunayo wajibu wa kuwatunza ninyi na mjione hii nchi inawatambua,hivyo basi nawasihi mpokee hivi vitambulisho mkavitunze viweze kuwasaidia katika matibabu yenu.Nataka kuwahakikishia serikali imejipanga kuhakikisha huduma za afya kwenu  wazee ni bure,ukiugua chukua kitambulisho chako nenda ukatibiwe bure."  alisema Mwaisumbe.

Nae afisa Ustawi jamii Wilaya ya Longido  Bi. Atuganile chisunga ambaye ndiyo mratibu wa zoezi hilo alisema, "kwa kuanzia tumeanza na kata ya Longido na tunajipanga kuendelea na zoezi la  kugawa vitambulisho vya Matibabu kwa Wazee wa wilaya nzima ya Longido  kwa sababu tunawathamini sana wazee wetu kwani bila wao wazee sisi tusingekuwa hapa leo na hata nchi yetu isingefika hapa tulipo hivyo wazee ni hazina yetu kubwa sana na mna kila sababu ya kupata vitambulisho hivi na nitahakikisha wazee wote wa Wilaya hii ya Longido wanapata Vitambulisho vya kupatiwa matibabu bure".

Wazee hao nao wameshukuru kwa kupewa vitambulisho vya matibabu na kuishukuru serikali ya Rais John Pombe Magufuli kwa kutambua uwepo wao."Tunashukuru kwa serikali hii ya Mh Rais kwa kutambua uwepo wetu mimi kama mzee nimekuwa nikisumbuka hata kama nikipata homa inagharimu kuanza kutafuta hela ya kununua dawa lakini kwa kupewa kitambulisho hiki nina hakika tatizo langu litamalizika kabisa nishukuru sana serikali namshukuru Rais wetu mtetezi wa wanyonge anatupenda sisi wazee na mshukuru mkuu wetu wa wilaya" alisema Bibi Maria ole Karooi mwenye umri wa miaka 90.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM