• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

WWF YAWANOA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU SERA YA UTUNZAJI MAZINGIRA LONGIDO

Posted on: October 15th, 2025

NA ABRAHAM NTAMBARA

Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira na Wanyamapori (WWF) limetoa mafunzo kwa Viongozi wa Dini, Vijiji na viongozi wa Kimila kuhusu Sera mbalimbali za utunzaji wa mazingira wilayani Longido.

Akizungumza katika mafunzo hayo ya siku tatu yaliyoanza leo Oktoba 15, 2025 wilayani Longido chini ya Mradi wa Faith4Restoration, Kiongozi wa Mradi huo kutoka WWF Prof. Noah Sitati alisema ni kwa mara ya kwanza wanatumia viongozi wa dini katika kuelemisha utunzaji wa mazingira.

Profesa Noah amesema Kwamba wameamua kuwatumia viongozi hao, kwasababu wamekuwa wakaeneza injili, hivyo anaamini itakuwa ni rahisi kupenyeza elimu ya utunzaji wa mazingira kwa waumini wao.

Alisema elimu hiyo wameanza kuitoa katika Vijiji vitatu ambavyo ni Orbomba, Kimokouwa na Eworendeke, hata hivyo alibainisha kuwa baadaye wataipeleka katika vijiji vingine.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi Faith4Restoration kutoka WWF Ofisi ya Arusha Jane Shuma alisema wanawapa mafunzo hayo kwasababu wao ndio watakaoshiriki katika utekelezaji wa mradi.

"Lengo la kuwashirikisha Viongozi wa Dini, Vijiji na Kimila ni kuhakikisha wanatoa mchango katika suala la utunzaji wa mazingira," alisema Shuma.

katika mafunzo hayo watawapitisha kwenye maeneo matatu ambayo ni kuhusu uondoshaji wa mimea vamizi, utunzaji wa vyanzo vya maji na mmomonyoko wa udongo uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Naye Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido Bi. Sofia Gashomba, alisema Longido kwa sehemu kubwa imeathiriwa na mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukame, hivyo mafunzo hayo yatasaidia katika utunzaji wa mazingira.

Kwamba viongozi hao watasaidia kutoa elimu kwa wananchi ili kuendelea kutunza mazingira kwa kuacha kukata miti na uchomaji mkaa hali ambayo itasaidia kurejesha uoto wa asili.

Aidha Sheikh wa Wilaya ya Longido Ramadhani Mpangala aliishukuru WWF kwa kuwashirikisha katika mafunzo hayo ya utunzaji wa mazingira.

Sheikh Mpangala alisema hata Dini inasema kuwa mazingira ni uhai, hivyo elimu wanayoipata kwenye Semina hiyo, wataipeleka kwa waumini wao.

Kadhalika Kiongozi wa Kimila na Mwenyekiti wa Nyanda za malisho Kijiji cha Eorendeke Lucus Sambeke alisema mafunzo ambayo wamekuwa wakipatiwa yamekuwa na faida kubwa kwani yameshaanza kuleta matokea kwa kuanza kurejesha uoto wa asili.

Alisema kuwa kama vingozi wamekuwa wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi ya utunzaji wa mazingira kwa kuwataka kuacha kukata mita na kuwahimiza kupanda miti.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • WWF YAWANOA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU SERA YA UTUNZAJI MAZINGIRA LONGIDO

    October 15, 2025
  • COMPASSION NA SERIKALI WAUNGANA KUMWEZESHA MTOTO WA KIKE NAMANGA

    October 13, 2025
  • SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S YAUNGA MKONO MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA, YAFUNGA MFUMO WA GESI

    October 14, 2025
  • SERIKALI YAAHIDI KUMALIZA KERO YA MAJI SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S IFIKAPO JANUARI 2026

    October 14, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.