• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

AHADI YA VIONGOZI WA MILA JUU YA UANDIKISHAJI WA ORODHA YA MPIGA KURA WILAYANI LONGIDO.

Posted on: October 16th, 2024

AHADI YA VIONGOZI WA MILA (MALAWAGWANANI) KWA MKUU WA WILAYA YA LONGIDO KUHUSU KUTOA ELIMU NA HAMASA KWA JAMII YA WAFUGAJI KUHUSU KUJIANDIKISHA KWENYE ORODHA YA MPIGA KURA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.


Viongozi wa mila (Malawagwanani) wilayani Longido wameahidi kutoa elimu na hamasa kwa jamii ya wafugaji katika jitihada za kuhakikisha ushiriki wao katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024. Ahadi hii ilitolewa mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe.Salum Kalli, alipokutana na viongozi hao kujadili mikakati ya kuhamasisha jamii ya wafugaji kujisajili kwenye orodha ya wapiga kura.


Katika mkutano huo, viongozi wa mila walieleza dhamira yao ya kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu juu ya umuhimu wa kujiandikisha na kushiriki kwenye uchaguzi, wakisema kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha demokrasia na kuhakikisha kuwa jamii yao inapata uwakilishi sahihi.Aidha viongozi hao Waliahidi kutumia mamlaka yao ya kijamii kushawishi na kuwahimiza wafugaji kuchukua jukumu la kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za mitaa wa tarehe 27 octoba 2024 kwa kuanza na hatua ya kujiandikisha.


Zoezi la uhamasishaji litaanza rasmi mara tu wataporejea kwenye maeneo yao ya utawala , na tayari viongozi hao wamekwishaanza kuhamasisha jamii kushiriki zoezi hilo muhimu. Malaigwanani hao Wamesema kuwa watapita kwa jamii na kwenye maeneo mbalimbali ili kufikisha ujumbe huu kwa wafugaji kwa njia zinazoeleweka na kuendana na maisha yao ya kila siku.


Mwenyekiti wa Malawagwanani wilaya, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kutambua mchango wao katika jamii na kuahidi kumpa ushirikiano wa dhati katika kukamilisha zoezi hilo ili lifanikiwe kwa asilimia mia moja. Aliongeza kuwa viongozi wa mila wataendelea kushirikiana na serikali kwa ukaribu katika kuhakikisha kila mfugaji anapata nafasi ya kujiandikisha na kushiriki katika uchaguzi huo muhimu kwa maendeleo ya wilaya ya Longido.


Mkuu wa Wilaya ya Longido alitoa shukrani zake kwa viongozi hao kwa kuonyesha nia ya dhati ya kushirikiana na serikali katika kuhamasisha jamii. Alisisitiza kuwa ushiriki wa jamii ya wafugaji ni muhimu kwa maendeleo ya wilaya na taifa kwa ujumla, na uchaguzi wa serikali za mitaa ni fursa nzuri ya kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata nafasi ya kushiriki katika maamuzi ya maendeleo ya eneo lake.

Kupitia ushirikiano huo, viongozi wa mila na serikali ya wilaya ya Longido wanaamini kuwa watafanikiwa kuongeza idadi ya wafugaji watakaojiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura, hivyo kuwezesha ushiriki wao kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM