• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

Huduma zetu-Utalii

 Wilaya ya Longido ni miongoni mwa wilaya sita (06) za Mkoa wa Arusha, kaskazini mwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jina “Longido” limetokana na Mlima Longido, ambao kwa lugha ya Kimasai huitwa Loongiito, likimaanisha “mlima wenye mawe ya kunolea visu.” Wilaya hii ina eneo la kilomita za mraba 8,180.

Kijiografia, Wilaya ya Longido imezungukwa na mifumo mikubwa ya ikolojia inayochangia umuhimu wake kama mazalia, malisho na mapito ya spishi mbalimbali za wanyamapori. Upande wa mashariki inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA) iliyounganishwa na Ushoroba wa Kimataifa wa Kitenden (Kitenden Wildlife Corridor). Kusini inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Arusha (ANAPA), magharibi na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) pamoja na Pori la Akiba la Pololeti, huku kaskazini ikipakana na Hifadhi ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya.

Mbali na mandhari yake ya kipekee, Wilaya ya Longido imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, vikiwemo spishi zaidi ya 40 za wanyamapori, aina mbalimbali za ndege wakiwemo Heroe wadogo (Lesser Flamingo) wenye mazalia Ziwa Natron, Mbuni (Ostrich), Tandawala (Kori Bustard) na Ndege Sekretari (Secretary Bird) pamoja na urahisi wa kufikika maeneo mengi ya vivutio. Mchanganyiko huu wa rasilimali na fursa unaiweka Longido katika nafasi ya kipekee kama kitovu cha shughuli za utalii kaskazini mwa Tanzania.

        Jedwali Na.1. Baadhi ya wanyamapori wanaopatikana Wilayani Longido.


Jina la kawaida
Spishi
Tembo
Loxodonta Africana
Nyati
Syncerus caffer
Twiga
Giraffa Camelopardalis
Simba
Panthera leo
Duma
Acinonyx jubatus
Chui
Panthera pardus
Mbwa Mwitu
Lycaon pictus
Digidigi
Madoqua kirkii
Pofu
Tragelaphus oryx
Mbuzi mawe
Oreotragus oreotragus
Swala pala
Aepyceros melampus
Swala Granti
Grant    gazelle
Tandala kubwa
Tragelaphus strepsiceros
Tandala mdogo
Tragelaphus imberbis
Choroa
Fringed Eared Oryx
Mbuni
Struthio camelus
Fisi madoa
Crocuta crocuta
Fisi Mraba
Hyaena hyaena
Swala thomi
Eudorcas thomsonii
Ngiri
Phacochoerus africanus
Nyumbu
Connochaetes taurinus
Pundamilia
Equus quagga
Swala Twiga
Litocranius walleri
Kori Bustard
Ardeotis kori
Heroe wadogo (Lesser Flamingo)
Phoeniconaias minor


Uwindaji wa Kitalii (Tourist Hunting):

Hii ni aina ya uvunaji wa wanyamapori madume yaliyozeeka unaofanywa na Wawindaji Wageni chini ya usimamizi wa Serikali kwa lengo la Utalii (Consumptive Wildlife Utilization). Mgeni anapaswa kulipia ada ya vibali na wanyama kupitia Kampuni inayomiliki Kitalu husika cha Uwindaji kabla ya kusafiri kutoka nchi yake kuja nchini Tanzania kwa Shughuli za Uwindaji. Aina hii ya Uwindaji, inafanyika katika maeneo maalum yaliyotengwa na Serikali kama vitalu vya Uwindaji kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii. Aidha, mwishoni mwa mwaka 2022, Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mnada wa Kielectroni (Electronic Auctions), iligawa Vitalu saba (07) vya Uwindaji Wilayani Longido kwa Kampuni sita (06) za Uwindaji kama inavyosomeka kwenye Jedwali Na.2. hapo chini.

Jedwali Na.2. Orodha ya Vitalu vya Uwindaji Wilayani Longido na Kampuni zinazomiliki. 

 

S/N
JINA LA KITALU
KAMPUNI INAYOMILIKA
MUDA WA UMILIKI

Pori Tengefu Ziwa Natron Kaskazini.
Adam Clements Safaris Ltd.
2023 - 2032

Pori Tengefu Ziwa Natron Kusini.
Robin Hurt Safaris Ltd.
2023 - 2032

Pori Tengefu Ziwa Natron Magharibi.
Kilombero North Safaris Ltd.
2023 - 2032

Pori Tengefu Ziwa Natron Mashariki.
Green Mile Safaris Co. Ltd
2023 - 2042

Pori Tengefu Longido Kaskazini.
Michel Mantheakis Safaris Ltd
2023 - 2032

Monduli Juu Open Area.
Tanzania Big Game Safaris Ltd.
2023 - 2032

Eneo la Uwindaji la Engasurai-EWMA
Kilombero North Safaris Ltd.
2023 - 2032

Utalii wa Picha (Photographic Tourism):

Hii ni aina ya utalii usio wa uvunaji (Non-Consumptive Wildlife Utilization) unaofanywa na wageni kwa kutembelea vivutio vya Utalii ndani ya Wilaya yetu kwa lengo la kupiga picha na kutazama wanyamapori katika mazingira yao. Wageni wengi hufika Longido kutazama Wanyamapori mbalimbali na ndege pamoja na kupanda mlima Longido wenye urefu wa mita 2,637 kujionea mandhari tambarare za mbuga zinazozunguka Mlima Kilimanjaro na Meru.

Utalii wa Kitamaduni (Cultural Tourism): 

Longido ni kitovu cha Utalii wa Kitamaduni ambapo wageni wanaweza kutembelea maboma ya Wamasai kwa Lengo la kujifunza kuhusu mila, tamaduni na maisha ya kila siku ya Jamii ya Wamasai. Wageni wataweza kupata fursa ya kupiga picha ya matukio halisi ya jamii hiyo kama wanawake wakiokota kuni, watoto wakichunga mifugo, na usanifu wa kipekee wa boma za Wamasai (nyumba za makazi).



Kwa maelezo na msaada zaidi fika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Longido, au

 piga simu namba :

 0784889889 Afisa Wanyamapori Wilaya,

 0787115234 Afisa Utalii Longido.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WILAYA YA LONGIDO WATOA TAMKO JUU YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 23, 2025
  • WANAFUNZI 5,188 KUFANYA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE LONGIDO

    October 21, 2025
  • WWF YADHAMIRIA KUREJESHA MAZINGIRA ASILIA YA LONGIDO

    October 20, 2025
  • MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA PILI YA MAFUNZO YA WWF KWA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA LONGIDO

    October 16, 2025
  • View All

Video

KAMATI YA AMANI NA HAKI WILAYANI LONGIDO YATOA TAMKO LA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.