• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO WAMEFANYA MKUTANO KUJADILI RASIMU YA MKATABA WA UTEKELEZAJI WA BIASHARA YA HEWA YA UKAA BAINA YA KAMPUNI YA SOIL FOR FUTURE NA VIJIJI TISA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO .

Posted on: May 4th, 2024

Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa J K Nyerere Tarehe 05/04/2024.

Akifungua mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido Mheshimiwa Simon Oitesoi amewataka wawekezaji hao kutoa Elimu ya kutosha kwa wajumbe ili kuwasaidia kuwa na Elimu thabiti kabla hawajakaa mezani na kusaini mkataba huo.


"Kwa kuwa biashara hii kwetu ni mpya niwaombe mtengeneza mazingira mazuri ya sisi kutoka ili tukajifunze kwa waliofanya, na sisi tuwe na uelewa wa pamoja kwa sababu kwetu katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido ni mpya tumesikia maeneo mengine wanafanya biaahara kama hii ila sio kwenye udongo sasa ili tuwe na uelewa mzuri tukajifunze kwa waliofanya kwanza "Alisema Mhe Oitesoi.


Akiwasilisha Rasimu ya Mkataba huo Mwanasheria wa Halmashauri Ndugu Dominic Ruhamvya amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa kwa kuwa bado ni Rasimu imeletwa mezani ili ijadiliwe na hatimae baraza liamue na kufanya maamuzi yaliyo sahihi juu ya Matumizi bora na sahihi ya Ardhi hasa kwenye maeneo ya Malisho ambapo Longido inalisha wanayama wa kufuga na Wanyama wasiofungwa.


Vile vile Bwana Ruhamvya amewaleza wajumbe kuwa Mradi huu haukusudii tu kukuza uendelevu wa mazingira bali pia kuimarisha uhamishaji wa teknolojia na maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii kwa kuzalisha na kugawana mapato yanayotokana ma mauzo ya viwango vya kaboni ambayo yanaweza kutumika kutoa huduma za kijamii ikiwa ni pamoja na mazingira safi, yenye afya na endelevu na kuboreshwa kwa huduma za kijamii.


Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido Ndugu Nasorro Shemzigwa amesema kwamba iwapo tutafikia muafaka juu ya usainishwaji wa Mkataba huu wa biashara ya hewa ya Ukaa mbali tu na kupata mapato, pia itasaidia sana kwenye utunzaji wa mazingira yetu, kwetu sis, kwa mifugo na wanyama wetu.


Sambamba na kuiomba Kampuni juu ya utoaji wa Elimu ya kutosha kw a wajumbe, pia amewaasa wajumbe  hao kutoa Elimu ya kutosha kwa jamii juu ya uwekezaji huu wa Hewa ya ukaa waelezwe kuhusu faida zitakazo patikana kutokana na utunzaji wa mazingira.


Tafadhali niwaombe wawekezaji watupeleke darasani tukajifunze tujua kwa wenzetu waliokwisha anza kufanya biashara hii iwe ndani ama nje ya nchi ya Tanzania. "Alisema Mheshimiwa Abel Njipai Diwani wa Noondoto.

Rasimu ya Mkataba huu imeainisha madhumuni ya Mkataba, masharti ya awali tarehs na muda, mgawanyo wa gharama na faida, taarifa za fedha na matumizi y a faida, Msamaha, Mkataba mzima, Uhalali, Taarifa, Sheria inayotumika, Ukomo wa Mkataba, majanga ya Asili,pamoja na Usuluhishi wa migogoro.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KAZI IENDELEE

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM