• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA MHE. NURDIN BABU AMEKUTANA NA KAMATI YA MSINGI YA AFYA YA JAMII KUTOA ELIMU YA UVIKO-19 NA UMUHIMU WA CHANJO YA UVIKO-19

Posted on: September 27th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Longido Mkoa wa Arusha Mhe. Nurudin Babu amekutana na kufanya majadiliano na viongozi wa Mila( Alaigwanani) pamoja na viongozi wa madhehebu mbalimbali (dini) juu ya kuhakikisha wananchi wilayani hapa wanapata chanjo ya UVIKO 19.

Alisema Kumekuwa na baadhi ya wawakilishi wa wananchi kupotosha jamii dhidi ya chanjo inayoendelea kutolewa ya Johnson and Johnson (JANSSEN) na kupelekea wananchi kuingiwa na hofu na kukata kuchanja.

" Hakuna serikali duniani ipo kwa ajili ya kuua wananchi wake,na hata hapa kwetu Tanzania hakuna Kiongozi Yupo tayari kuua wananchi wake hivyo achaneni na Maneno ya wapotoshaji" alisema

Aidha alitoa angalizo kwa baadhi ya viongozi wenye tabia hiyo kuacha Mara moja kwani atawachukulia hatua Kali za kisheria ,huku akitoa agizo kwa wakuu wa idara ya elimu na afya kuhakikisha watumishi wote wa idara  hizo wanapata chanjo ili kuwalinda watu na wanafunzi wanaowahudumia au kuwafundisha.

Naye Kaimu Mkurugenzi Ndugu Edward Mboya alimuhakikishia Mkuu wa wilaya kuwa atahakikisha maagizo yote aliyotoa yanatekelezwa kwa wakati kabda ya zoezi hili kuisha kwa kuwahimiza watumishi wote wanaotoa huduma kwa jamii wanafuata taratibu zote za kujikinga na ugonjwa wa Korona UVIKO-19 na kuhakikisha wanapata chanjo ya UVIKO-19 hasa walimu na wahudumu wa afya.

Baadi ya wazee wa Mila walitoa maoni yao na kuzungumzia sababu ya jamii kukataa au kuogopa kuchanja ni Maneno dhidi ya chanjo hiyo kuwa inapunguza nguvu za kiume lakini pia tatizo kubwa ni jamii kukosa elimu dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19.

Hata hivyo viongozi hao wa Mila waliazimia kwa pamoja kuwa sauti ya jamii katika kukubali na kupokea chanjo hiyo,huku wakikiri kuwa ugonjwa huo upo na umeua watu wengi Sana hata ndani ya jamii na kumuahidi Mkuu wa wilaya kuwa watasaidia kueneza elimu juu ya umuhimu wa kupata chanjo kwenye jamii wanazotoka.

Kwa upande wao viongozi wa dini walisema watatoa elimu katika nyumba za ibada na kukemea vitendo vya baadhi ya viongozi wa dini wanaopotosha wananchi juu ya chanjo na kusema masuala yanayohusiana na afya waachiwe wataalamu wa afya wao wabaki na mambo ya kiimani.


Naye Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt  Seleman Mtenjela alisema chanjo hiyo ni salama na wamefanikiwa kuchanja watu 867 sawa na asilimia  33 ya dozi iliyotolewa wilayani hapo,hata hivyo Kati ya hao waliopata chanjo hakuna aliyewahi kutoa taarifa Kama amepata madhara au kuwepo kwa taarifa za vifo.

" Maudhi madogo madogo yapo lakini ni ya kawaida kutokana na kitu kipya kinavyoingia mwilini, ikiwemo maumivu kiasi katika sehemu uliyochomwa sindano,uchovu,homa au baridi na maumivu ya kichwa" alisema.

Baadhi ya wananchi waliochoma chanjo hiyo wamekanusha uvumi kuhusu kupotea kwa nguvu za kiume na kusema wapo imara ,huku wengine wakisema hawajapata madhara yoyote ya kiafya.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM