• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC LONGIDO AFUNGUA KIKAO CHA WATAALAMU WA AFYA CHA KUJADILI VIFO VINAVYOTOKANA NA UZAZI NA WATOTO WACHANGA

Posted on: November 13th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli, ametoa wito kwa watumishi wa huduma za afya kote nchini kutumia lugha nzuri na yenye staha wanapohudumia wateja wanaofika kwenye vituo vya afya. Akizungumza wakati wa kufungua kikao kazi cha Mkoa kilichojadili vifo vinavyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga, kilichofanyika katika ukumbi wa J.K. Nyerere Wilayani Longido, Mheshimiwa Kalli alisisitiza umuhimu wa mawasiliano mazuri kati ya watoa huduma na wagonjwa.

“Lugha nzuri ni sehemu muhimu ya huduma bora kwa wateja. Inasaidia kujenga imani, kupunguza hofu, na kuongeza ufanisi wa huduma zinazotolewa. Nawataka watumishi wote wa sekta ya afya kote nchini kuelewa kwamba wagonjwa wanapofika katika vituo vya afya, wanahitaji si tu matibabu bali pia faraja na heshima,” alisema Mheshimiwa Kalli.

Kikao hicho kilikusanya wataalamu wa afya, viongozi wa serikali, na wadau mbalimbali ili kutathmini changamoto na suluhisho za kudhibiti vifo vya mama na mtoto. Mheshimiwa Kalli aliwataka washiriki kuhakikisha kwamba mbinu za kuboresha huduma zinatiliwa mkazo, ikiwa ni pamoja na kuboresha mawasiliano na wagonjwa.

“Ni jukumu letu wote kuhakikisha kuwa huduma za afya zinaboreshwa kwa kila njia, na hilo linaanza na jinsi tunavyowasiliana na kuwahudumia wateja wetu,” aliongeza.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Simon Oitesoi, amewataka washiriki kuzingatia mafunzo hayo yatakayotolewa na wawezeshaji ili kuleta matokeo chanya katika huduma ya afya.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Nassoro Shemzigwa, amepongeza juhudi za Idara ya Afya kwa kuchagua Longido kama mwenyeji wa mafunzo hayo muhimu. Bw. Shemzigwa alieleza kwa furaha kuwa, “Ni heshima kubwa kwa Wilaya yetu kuwa mwenyeji wa mafunzo haya. Nawakaribisha kwa mikono miwili na nina matumaini kuwa maarifa mtakayoyapata yatachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za afya kwa wananchi wetu.”

Kikao hiki kinatarajiwa kuleta matokeo chanya katika kuboresha huduma za afya na kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi na watoto wachanga katika Mkoa wa Longido na maeneo mengine nchini.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM