• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

Posted on: May 14th, 2025


Na Hapiness Nselu 


MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Nassoro Shemzigwa, amefungua mafunzo ya siku moja kwa ajili ya waandishi wasaidizi na waendeshaji wa mashine za BVR, yatakayofanyika katika kata zote 18 za wilaya hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya awamu ya pili ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Julius Kambarage Nyerere uliopo makao makuu ya halmashauri hiyo, Bw. Shemzigwa aliwapongeza washiriki kwa kuaminiwa na kuteuliwa tena kushiriki katika utekelezaji wa jukumu hilo muhimu la kitaifa.


Zoezi la uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura linatarajiwa kuanza rasmi Mei 16 hadi 22, 2025, katika kata zote 18 za Wilaya ya Longido.


“Mnatakiwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu, kutunza vifaa mlivyopewa, kuepuka vitendo vya uzembe au visivyofaa vinavyoweza kuhatarisha mchakato huu muhimu. Fanyeni kazi kwa weredi kwa kuzingatia sheria na kanuni za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi,” alisisitiza Mkurugenzi.


Amesema lengo ni kuhakikisha kila mwananchi mwenye sifa anapata haki yake ya msingi ya kupiga kura na kuchagua viongozi anaowataka katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Serikali Kuu.


Kwa upande wake, Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Longido, Bw. Nevviling Lymo, alisema ofisi yake itahakikisha inasimamia kwa karibu utekelezaji wa zoezi hilo ili lifanikishwe kwa viwango vya juu na kwa wakati uliopangwa.


“Ni wajibu wa kila afisa mwandikishaji kuhakikisha taarifa zote muhimu zinawasilishwa kwa wakati na mahali sahihi, na kushirikiana kikamilifu na watendaji walioko vituoni ili kufanikisha kazi hii,” alisema Bw. Lymo.


Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo, *Mwenyekiti wa Mafunzo, Bw. Ernest Lotakajack , alisema wako tayari kuhakikisha zoezi linafanyika kwa ufanisi mkubwa na kuleta matokeo chanya katika jimbo hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM