• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO IMEFANYA KIKAO KAZI CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE .

Posted on: November 11th, 2024

Na Happiness Nselu



Kikao kazi cha tathmini ya lishe kilichofanyika leo katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Longido, kikiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Salum Kalli.


Katika kikao hicho, Mheshimiwa Kalli alisisitiza umuhimu wa lishe bora kwa jamii, akieleza kwamba afya ya mama na mtoto inategemea sana mlo kamili na usawa. Alisisitiza pia kuwa, ni muhimu kwa kina baba kushiriki kikamilifu katika kujenga afya ya familia zao, hususan katika kuhakikisha mlo bora kwa wake zao na watoto wao.


Afisa Lishe wa Wilaya Bi. Adelina Kahija alisoma tathmini ya lishe katika wilaya, akionyesha mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto zinazohitaji kushughulikiwa ili kuboresha lishe kwa jamii. Aliwahimiza viongozi na wananchi kuongeza jitihada za kutoa elimu zaidi kuhusu mlo bora, ili kupambana na utapiamlo na magonjwa yanayotokana na lishe duni.


Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Deoniz Mathew Majani, alitoa shukrani kwa wajumbe wa kikao hicho kwa kazi yao ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa mlo kamili.


Alisisitiza kuwa jamii inahitaji kuendelea kuwa na uelewa wa juu kuhusu lishe bora na akasema kwamba ni muda sasa wa kuhamasisha jamii kuhusu hatari ya wamama kujifungulia nyumbani, na umuhimu wa kujifungulia katika vituo vya afya kwa usalama wa mama na mtoto.


Aidha, Dkt. Deoniz Mathew Majani alizungumza kuhusu huduma ya "M-Mama" inayotolewa na Serikali ambayo ni huduma ya usafirishaji wa wamama wajawazito na watoto wenye mahitaji maalum kutoka vijijini hadi vituo vya afya.


Alisisitiza kuwa huduma hii ni muhimu kwa afya ya mama na mtoto, na alitoa wito kwa watendaji wa kaya na vijiji kuwa na madereva jamii watakaorahisisha upatikanaji wa huduma hii kwa haraka na ufanisi. Alisema kuwa ni muhimu kuhakikisha kwamba huduma za usafiri zipo karibu na wananchi, ili kuepusha vifo vya uzazi na madhara yanayoweza kutokea kutokana na ucheleweshaji wa huduma za afya.


Kikao hicho kilihudhuriwa na watumishi wa Halmashauri pamoja na  watendaji wa serikali, na kililenga kuimarisha ushirikiano wa pamoja katika kuhakikisha wilaya ya Longido inakuwa na lishe bora na huduma bora za afya kwa wote.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM