• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Posted on: August 7th, 2025

Na Happiness Nselu

 Halmashauri ya Wilaya ya Longido imeadhimisha Wiki ya Unyonyeshaji tarehe 7 Agosti 2025 kwa mafanikio makubwa kupitia sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Eorendeke, Kata ya Kimokouwa, na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi, watoa huduma za afya na viongozi wa jamii.


Maadhimisho hayo, yaliyolenga kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa watoto wachanga na lishe bora kwa familia, yalipambwa na uwepo wa Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli, ambaye alikuwa mgeni rasmi.


Mganga Mkuu wa Wilaya, Dk. Methew Majani, akisoma risala rasmi, alieleza dhamira ya halmashauri katika kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto. Alisisitiza kuwa unyonyeshaji sahihi unalinda afya ya watoto wachanga, unapunguza vifo vya watoto na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla.


Afisa Lishe wa Wilaya, Bi Adelina Kahija, alitoa elimu kwa kina kwa kina mama na walezi kuhusu umuhimu wa kunyonyesha ndani ya saa moja baada ya kujifungua, unyonyeshaji wa pekee kwa miezi sita ya mwanzo, na kuhakikisha familia inapata mlo kamili wenye virutubisho muhimu.


“Tunataka kila kaya hapa Longido ifahamu kuwa unyonyeshaji ni msingi wa kizazi chenye afya, na lishe bora ni jukumu la familia nzima,” alisema, akihimiza wanaume kushirikiana na wake zao katika jukumu hilo.


Sherehe hizo zilipambwa na burudani kutoka kikundi cha muziki cha ACE Group, kilichotumbuiza kwa nyimbo zenye ujumbe wa kuhamasisha unyonyeshaji, malezi bora ya mama na mtoto, pamoja na ulaji wa chakula chenye virutubisho.

Mheshimiwa Kalli alisifu waandaaji na wadau kwa jitihada zao, akiwataka wananchi kuyatumia mafunzo yaliyotolewa. “Mama mwenye afya analea mtoto mwenye afya, na mtoto mwenye afya anajenga taifa imara,” alisisitiza.


Wiki ya Unyonyeshaji huadhimishwa duniani kote kila mwaka katika wiki ya kwanza ya Agosti, huku kaulimbiu ya mwaka huu ikisema "THAMINI UNYONYESHAJI ;WEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA MAMA NA MTOTO".


@ortamisemi@wizara_afyatz@rc_mkoa_arusha@ikulu_mawasilian

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    August 07, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WILAYANI LONGIDO WALA KIAPO CHA UADILIFU

    August 05, 2025
  • SHIRIKA LA MONDO TANZANIA LAKABIDHI MAGODORO 32 KWA WANANFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU SHULE YA MSINGI LONGIDO

    July 30, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • View All

Video

LONGIDO YASHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE MAONESHO YA NANE NANE YANAYOFANYIKA VIWANJA VYA THEMI - NJIRO ARUSHA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.