• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YABORESHA HUDUMA KWA WANANCHI KWA KUGAWA PIKIPIKI KWA MAAFISA WA IDARA YA AFYA NA MAENDELEO YA JAMII

Posted on: November 20th, 2024

Na Happiness E Nselu


Katika juhudi za kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido imekabidhi pikipiki nne kwa maafisa wa Idara ya Afya na Maendeleo ya Jamii. Hatua hii inalenga kurahisisha utendaji kazi wa maafisa hao kwa kuwafikia wananchi walioko maeneo ya vijijini, hususan maeneo yenye changamoto za kijiografia.  


Akikabidhi pikipiki hizo, Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli, aliishukuru ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa kujali mahitaji ya idara hizo na kuonyesha dhamira ya kuimarisha huduma kwa wananchi. Aidha, Mheshimiwa Kalli alimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuboresha sekta za afya na maendeleo ya jamii, ambazo zimewezesha upatikanaji wa nyenzo hizo muhimu.  


Mheshimiwa Kalli aliwataka maafisa waliopokea pikipiki hizo kuhakikisha wanazitumia kwa malengo yaliyokusudiwa, akisisitiza kwamba hazipaswi kutumika kwa shughuli binafsi kama vile bodaboda au biashara nyingine. "Pikipiki hizi ni kwa ajili ya wananchi. Tutawafuatilia kuhakikisha zinatumika ipasavyo katika kutoa huduma bora kwa jamii," alisema.  


Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Bi. Grace Mghase, Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya, alisema kuwa pikipiki hizo ni sehemu ya jitihada za halmashauri ya kuhakikisha huduma muhimu zinawafikia wananchi kwa urahisi na kwa haraka. “Nyenzo hizi zitatusaidia kufanikisha malengo yetu ya kuwafikia wananchi hata katika maeneo yaliyo mbali,” alisema Bi. Mghase.  


Afisa Afya wa Wilaya, Bi. Judithi Meela, alitoa shukrani kwa ofisi ya mkurugenzi kwa kuwezesha upatikanaji wa pikipiki hizo muhimu. Alisema kuwa pikipiki hizo zitakuwa mkombozi mkubwa kwa maafisa wa idara ya afya katika kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi kwa wakati na kwa ufanisi zaidi.  


Naye Bw. Musa Kabula Afisa maendeleo ya jamii, aliyepokea pikipiki hizo kwa niaba ya maafisa wa Maendeleo ya Jamii, alisema kuwa nyenzo hizo zitawasaidia kufanikisha kazi zao katika maeneo yote ya wilaya. “Changamoto za miundombinu hazitakuwa tena kikwazo. Sasa tunaweza kuwahudumia wananchi wetu kwa wakati unaofaa,” alisema huku akitoa shukrani kwa uongozi wa halmashauri.  


Halmashauri ya Wilaya ya Longido inaendelea kuonyesha dhamira yake ya kuboresha maisha ya wananchi kwa kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kupitia uwekezaji wa rasilimali muhimu. Hatua kama hizi si tu zinaharakisha maendeleo ya kijamii bali pia zinaimarisha uhusiano kati ya serikali na wananchi wake.




Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM