• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

LIONS CLUB of ARUSHA, YASAIDIA WAGONJWA WA MACHO LONGIDO

Posted on: May 19th, 2019

 Shirika la LIONS CLUB of ARUSHA katika hatua ya kuendelea kusaidia watu waishio vijijini limetoa msaada wa huduma ya macho katika Hospitali ya Wilaya ya Longido  pamoja na kukabidhi miche ya Miti 70 kwa Afisa misitu wa Wilaya hiyo ili kuboresha utunzaji wa mazingira, Mei 19, 2019.

Akizungumzia zoezi la utoaji wa msaada huo Mkurugenzi wa Lions Club of Arusha Balwinder Singh Bansal amesema kuwa shirika linalenga kusaidia maeneo yote ya Vijijini katika mkoa wa Arusha yenye uhitaji katika Elimu, Afya, Mazingira na Ustawi wa jamii.

Vilevile Bansal amesema kuwa huduma ya macho itasaidia kuendelea kwa shughuli za hapa na pale kwa kiasi kukubwa hasa kwa wanachi ambao walikuwa hawaoni karibu na mbali “wananchi wataanza kuona vyema sasa maandishi, kuchambua vyakula n.k. na wale wasiokuwa na uwezo wa kununua miwani wamepatakulingana na matatizo walionayo baada ya vipimo kutoka kwa wataalamu” amesema Bansal

Ameendelea kusema kuwa Lions Club of Arusha inatambua uwepo wa watu kama hawa na itaendelea kuwasaidia kwa kadri iwezekanavyo na kutoa ushauri wa kitaalamu wa kufika Hospitali watakazoelekezwa mara kwa mara kwa matibabu zaidi wale wenye matatizo kama Mtoto wa jicho n.k., pia katika mazingira amefafanua kuwa Longido inakuwa na ukame kwahiyo watashirikiana kuumaliza.

Naye Mratibu wa Lions Club of Arusha Maswanya Yusuf ameelezea jinsi walivyotambua uwepo wa wananchi wenye nia ya kulitumikia taifa lakini hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu ni baada ya kuona waliowengi wanapatikana Vijijini. Ambapo katika zoezi hilo wamejitokeza wananchi wengi swala ambalo limepelekea zoezi kuanza asubuhi majia ya saa 03:00 mpaka 12: jioni.

Kwa upande wake Mratibu wa Macho Wilaya ya Longido Gustaph Thadeus Materu amesema lengo la huduma hii iliyotolewa na Lions Club of Arusha ni kupima macho na kutoa huduma kwa watakaogundulika na matatizo, na kwa wale watakaogundulika wana ugonjwa kama mtoto wa jicho watapata huduma katika hospitali ya St. Elizabeth vilevile watakaoshindikana watagharamikiwa gharama za matibabu katika Hospitali ya KCMC.

Materu amebainisha chanzo  cha magonjwa kama ya macho kuwa ni Uzee, Vumbi, maji machafu, kisukari n.k. Pia ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya hiyo kufika hospitalini hapo na kuonana na wataalamu kwa matibabu zaidi.

Akipokea miche ya miti 70 Afisa Misitu wa Wilaya ya Longido Boaz Mtokoma amewapongeza Lions Club of Arusha kwa msaada huo huku akiahidi kupanda miti hiyo kwa wakati katika maeneo mbalimbali “Kwa niaba ya mkurugenzi wa Wilaya nitoa shukrua za dhati kwenu na muendelee kutukumbuka tunaomba zaidi na zaidi bado tuna uhitaji mkubwa wa miche ndani ya Wilaya yetu” alisema Boaz

Boaz Mtokoma ameendelea kusema kuwa shukrani za dhati ziwafikie watu pamoja na mashirika binafsi na serikali kwa misaada ya miche ya miti inayoendelea kutoa wilayani Longido.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM