• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

LONGIDO YAAGA MADIWANI WAKE KWA HESHIMA, YASIFIA UONGOZI WAO WA HEKIMA NA BUSARA

Posted on: June 20th, 2025

Na Happiness Nselu – Longido

Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido umeonyesha kuthamini mchango wa viongozi wa Baraza la Madiwani waliomaliza muda wao, kupitia kikao kifupi cha kuagana kilichofanyika leo tarehe 20 juni 2025 katika ukumbi mdogo wa halmashauri hiyo.

Katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Simoni Oitesoi na Makamu Mwenyekiti Mhe. Peter Lekanet waliowakilisha Madiwani wengine, walipongezwa kwa uongozi wao wa hekima, busara na uwajibikaji uliosaidia kuleta mageuzi makubwa katika Halmashauri hiyo.

Kwa kipindi cha uongozi wao kuanzia mwaka 2020 hadi 2025, Halmashauri hiyo imefanikiwa kuongeza mapato ya ndani kutoka shilingi bilioni 1.5 hadi kufikia shilingi bilioni 5 kwa mwaka mchango ambao Menejimenti ya Halmashauri umeutambua kama wa kihistoria.

Akizungumza kwa niaba ya Madiwani wenzake, Mhe. Oitesoi alisema kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na ushirikiano wa karibu baina ya Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri. Alisisitiza kuwa wamefanya kazi kwa mshikamano na kuweka mbele maslahi ya wananchi wa Wilaya ya Longido.

Makamu Mwenyekiti Mhe. Peter Lekanet, kwa upande wake, alieleza kuwa uongozi wao ulilenga kuimarisha misingi ya amani, uwajibikaji na utulivu kazini ili kuwezesha watumishi kufanya kazi kwa bidii zaidi.

Nae, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Bw. Nassoro Shemzigwa, alitoa salamu za shukrani kwa niaba ya menejimenti, akiwahakikishia viongozi hao kuwa kazi waliyoifanya imeacha alama isiyofutika katika historia ya halmashauri hiyo.

Akizungumzia kuondoka kwao, Bw. Shemzigwa alisema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya maandalizi ya mchakato wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2025, na kwamba menejimenti inaichukulia kama mapumziko ya muda mfupi kwa viongozi hao.

“Kwa kweli tunaamini kwamba huu si mwisho, bali ni mapumziko ya muda. Ni matumaini yetu kama Menejimenti kwamba tutawaona tena, tukiendelea kushirikiana katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Halmashauri yetu,” alisema kwa matumaini.

Kwa ujumla, kikao hicho kimeacha taswira chanya ya mshikamano kati ya watumishi na viongozi waliomaliza muda wao, hali inayowapa matumaini wananchi wa Wilaya ya Longido juu ya mustakabali wa maendeleo ya wilaya yao.



Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    August 07, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WILAYANI LONGIDO WALA KIAPO CHA UADILIFU

    August 05, 2025
  • SHIRIKA LA MONDO TANZANIA LAKABIDHI MAGODORO 32 KWA WANANFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU SHULE YA MSINGI LONGIDO

    July 30, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • View All

Video

LONGIDO YASHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE MAONESHO YA NANE NANE YANAYOFANYIKA VIWANJA VYA THEMI - NJIRO ARUSHA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.