• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

LONGIDO YAANDAA BONANZA LA KUHAMASISHA UCHAGUZI WA SERIAKLI ZA MITAA WA TAREHE 27.11.2024

Posted on: November 19th, 2024

Msimamizi wa uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, ameandaa bonanza la uchaguzi  kwa lengo la kuhamasisha jamii na kuongeza uelewa kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024. Bonanza hili lilifanyika katika viwanja vya Halmashauri, vilivyopo karibu na Kituo cha Polisi Longido, ambapo timu za Longido Staff na Veteran FC zilipambana katika mchezo wa soka.


Katika mchezo huo, Veteran FC walionyesha umahiri wao na kuibuka na ushindi wa bao 2 kwa sifuri dhidi ya Longido Staff. Mchezo huu ulilenga kutoa fursa ya kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi, huku pia ukilenga kukuza umoja na mshikamano miongoni mwa vijana.


Akizungumza kwa niaba ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya, Bw. Nestory Dagharo, alisisitiza kuwa michezo ni njia bora ya kuhamasisha vijana kushiriki katika uchaguzi. Alisema, "Vijana ni nguvu ya Taifa, na Taifa linawategemea vijana ili liende mbele. Michezo ni njia bora ya kuhamasisha ushiriki wao katika shughuli za kijamii na uchaguzi wa serikali za mitaa."


Pia, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Bw. Elimeliki Ukwai, alitoa elimu kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwataka wananchi wa Wilaya ya Longido kutumia fursa ya uchaguzi wa tarehe 27 Novemba 2024 kwa kuelekea vituoni na kupiga kura ili kuchagua viongozi watakaowaongoza kwa maendeleo ya vijiji, kata, tarafa, na wilaya kwa ujumla. Alisisitiza kwamba kila raia ana wajibu wa kushiriki katika uchaguzi huo ili kuhakikisha uongozi bora na maendeleo ya maeneo yao.


Vilevile, Mchezaji wa Longido Staff, Bw. Steven, alieleza kuwa mechi hiyo ilikuwa na umuhimu mkubwa kwao, kwani ilileta umoja na mshikamano miongoni mwa vijana, hasa wa Tanzania. Alisema kuwa mchezo huu umekumbusha vijana wajibu wao katika kutumikia taifa na kuleta mabadiliko chanya kupitia ushiriki wao katika shughuli za kijamii, ikiwa ni pamoja na uchaguzi.


Bonanza hili limekuwa ni jukwaa muhimu kwa kuhamasisha wananchi, na hasa vijana, kutambua haki na wajibu wao katika michakato ya kisiasa na kijamii, ikiwa ni sehemu ya kujenga taifa lenye nguvu na umoja.

"SERIKALI ZA MITAA SAUTI YA WANANCHI JITOKEZE KUSHIRIKI UCHAGUZI".


LONGIDO TUTASHIRIKI 27 NOVEMBA 2024.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM