• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAHAKAMA YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA SHERIA KWA KUFANYA MATENDO YA HURUMA KWA WAHITAJI

Posted on: January 25th, 2025

Na Happiness Nselu 


Mahakama ya Wilaya ya Longido leo imefungua rasmi maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa mwaka 2025. Maadhimisho haya, ambayo yalianza rasmi tarehe 25 Januari 2025, yataendelea hadi tarehe 31 Januari 2025, yakiwa na kauli mbiu isemayo "Nafasi ya Taasisi Zinazosimamia Haki Madai katika Kufikia Malengo Makuu ya Dira ya Maendeleo."


Akizungumza kwenye ufunguzi wa maadhimisho hayo, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Longido, Hakimu Mfawidhi wa wilaya ya Longido. Mhe. ELIARUSIA REUBEN NASSARY Aliwataka wananchi na wadau wote wa sekta ya sheria  kuwa na uelewa zaidi kuhusu haki zao na umuhimu wa mifumo ya kisheria katika kufikia maendeleo endelevu. Aliwahimiza pia wataalamu na wataalamu wa sheria kushirikiana kwa karibu katika kutoa elimu na huduma kwa wananchi hasa wale walio katika maeneo ya mbali.


Katika hafla hiyo, wajumbe wa maadhimisho walipata fursa ya kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Longido, ambapo walitembelea wodi za wazazi na watoto. Katika ziara hiyo, walifanya matendo ya huruma kwa kutoa zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na sabuni, pampasi, mafuta na pesa taslimu kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo.


Pia, wajumbe walitembelea Nyumba Salama ya Wilaya ya Longido, ambapo walitoa elimu kuhusu haki za watoto na jinsi ya kupata msaada wa kisheria kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia, hususan katika jamii za kimasai. Walitoa mwanga kwa jamii kuhusu maeneo ambayo waathirika wanaweza kupata msaada wa kisheria, na umuhimu wa kuendelea kupigania haki za wanawake na watoto.


Akiongea kwa niaba ya serikali, Katibu Tawala wa Wilaya ya Longido, Rahma Kondo aliwashukuru watumishi wa mahakama kwa kujitoa kwao katika kutoa elimu na msaada kwa jamii yenye uhitaji. Alisema kuwa ni jambo jema na lenye manufaa kwa jamii, akisisitiza kuwa serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za sheria kutoa huduma kwa watu wanaohitaji msaada wa kisheria. Aliongeza kuwa jamii inapaswa kuacha kabisa vitendo vya ukatili vinavyofanywa dhidi ya watoto na wanawake, na kuwataka wananchi kufuata sheria na taratibu za kisheria pale wanapokumbana na changamoto hizo katika maeneo yao.


Kwa upande mwingine, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Longido, Dr Deoniz Methew Majani alitoa shukrani kwa timu kutoka Mahakama ya Wilaya ya Longido pamoja na viongozi wa serikali waliofika na kutoa elimu kwa watu waliokuwepo katika vituo hivyo, Hospitali ya Wilaya na Nyumba Salama. Alisema kuwa matendo ya huruma yaliyofanywa ni ya kuigwa na kutamaniwa na taasisi zote, na alitoa wito kwa taasisi za serikali na zisizo za serikali kufanya matendo kama haya ya huruma na msaada kwa jamii, ili kusaidia jamii isiyokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu haki zao na huduma za kisheria.


Maadhimisho ya Wiki ya Sheria ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa sheria na haki, huku wakizingatia kuwa sheria ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo ya taifa.




Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    August 07, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WILAYANI LONGIDO WALA KIAPO CHA UADILIFU

    August 05, 2025
  • SHIRIKA LA MONDO TANZANIA LAKABIDHI MAGODORO 32 KWA WANANFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU SHULE YA MSINGI LONGIDO

    July 30, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • View All

Video

LONGIDO YASHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE MAONESHO YA NANE NANE YANAYOFANYIKA VIWANJA VYA THEMI - NJIRO ARUSHA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.