• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YA MAJI KUKAGULIWA NCHI NZIMA

Posted on: April 11th, 2017

SERIKALI inafanya mapitio na kufanya uchunguzi wa miradi yote ya maji nchini ili kubaini inayofanya kazi na isiyofanya kazi.

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isack Kamwelwe alitoa uhakika huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mufindi Kusini, Menrad Kigola (CCM) aliyetaka kujua Serikali inafanyika nini kuboresha miradi ya maji iliyoanzishwa, lakini haifanyi kazi.

Alisema serikali inapitia miradi hiyo ikiwamo ya maji iliyojengwa Mufindi Kusini ambako matangi 11 yalijengwa, lakini hayana maji.

Naibu Waziri alisema mara uchunguzi huo utakapokamilika, mkakati wa Serikali utakuwa kuboresha miundombinu ya maji ikiwamo kusafisha matangi na visima vilivyochimbwa ambavyo havina maji ili kuhakikisha vinafanya kazi.

Akijibu swali la msingi la mbunge huyo aliyetaka kujua serikali itamaliza lini ujenzi wa mradi wa Maji Sawala, Mtwango, Lufuna na Kibao, Kamwelwe alisema mradi huo ulianza kutekelezwa Juni mosi, 2015 na ulitarajiwa kukamilika Juni mosi, mwaka jana.

Alisema utekelezaji wa mradi huo ulipangwa kufanyika kwa awamu tatu ambazo ni kujenga mahali pa kutega maji na kupeleka maji katika kijiji cha Sawala.

Awamu ya kwanza ya utekelezaji imefanyika katika kijiji cha Sawala kwa gharama ya Sh milioni 644.21 na hadi sasa Sh milioni 261.64 zimetumika katika mradi huo.

Kazi zilizotekelezwa hadi sasa ni pamoja na ujenzi wa mahali pa kuchukua maji, visima, boma za nyumbani na ulazaji wa bomba kuu, ujenzi wa tangi mita za ujazo 200 na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 16 na ehemu ya mabomba ya usambazaji kilometa 3.4 kwa wastani wa kazi umefanyika kwa asilimia 50 kwa kijiji cha Sawala tu.

Mradi huo haukukamilika kwa wakati kutokana na mkandarasi kushindwa kukamilisha kazi kwa mujibu wa mkataba.

Novemba mwaka huu, halmashauri ya wilaya ya Mufindi ilivunja mkataba na mkandarasi huyo, na kuamua kutangaza upya Februari 7, mwaka huu ili kumpata mpya.

Mkandarasi anatarajiwa kupatikana Juni mwaka huu, na kazi itakamilika katika mwaka huu wa fedha.


Chanzo Habari Leo. By Joseph P Mkumbwa

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM