• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

Posted on: April 17th, 2025

Na Happiness Nselu , Longido

Katika juhudi za serikali ya awamu ya sita kuhamasisha matumizi ya nishati safi na kuondokana na utegemezi wa nishati chafu kama kuni na mkaa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa msaada wa mitungi 50 ya gesi kwa mama na baba lishe wa Wilaya ya Longido.

Zoezi la ugawaji wa mitungi hiyo limefanyika kwa mafanikio makubwa na kuongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Salum Kalli, ambaye alikabidhi rasmi mitungi hiyo kwa wajasiriamali hao wadogo kama sehemu ya mpango wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi kwa ajili ya kuhifadhi mazingira na kuboresha afya za wananchi.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mhe. Kalli alisema kuwa dhamira ya Rais ni kuhakikisha kila kaya, hasa zinazojihusisha na shughuli za upishi, zinatumia nishati safi ili kuokoa mazingira na kupunguza athari za kiafya zitokanazo na moshi wa kuni na mkaa.

“Rais amedhamiria kuona Watanzania wanapika kwa usalama zaidi na kwa njia ya kisasa. Mitungi hii ya gesi si tu kwamba itarahisisha kazi zenu, bali pia ni mchango mkubwa katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira,” alisema Mhe. Kalli.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo, Bi Grace Mghase, alitumia fursa hiyo kuwahimiza wakazi wa Longido kuunga mkono juhudi za serikali kwa kubadilika kifikra na kuachana na matumizi ya nishati chafu.

“Hii ni fursa muhimu kwa jamii yetu. Tukiendelea kutumia kuni na mkaa, tunaharibu misitu na afya zetu pia ziko hatarini. Gesi ni njia salama, safi na ya haraka katika shughuli za kila siku, hasa kwa mama na baba lishe ambao muda ni rasilimali muhimu,” alieleza Bi Mghase.

Kwa upande wake, mama Saruni ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mama na Baba Lishe wilayani humo, alitoa shukrani kwa serikali kwa kuwakumbuka wafanyabiashara wadogo na kuwapatia vifaa vinavyowawezesha kuboresha huduma zao kwa wateja.

“Kwa kweli tumefurahi sana. Hatua hii ni ya kihistoria kwa sisi mama na baba lishe wa Longido. Tunaahidi kuzitumia mitungi hii kwa uangalifu, tukiwa na lengo la kuboresha huduma zetu na kuhakikisha wateja wetu wanapata vyakula bora kwa wakati,” alisema mama Saruni kwa furaha.

Wananchi waliohudhuria tukio hilo walionekana wenye hamasa kubwa huku wengi wakisema kuwa hatua hiyo imewapa mwanga kuhusu umuhimu wa kuhama kutoka kwenye matumizi ya kuni na mkaa kwenda kwenye nishati safi kama gesi, jua, na umeme wa uhakika.

Kwa mujibu wa Afisa Maendeleo ya Jamii, mpango wa ugawaji wa nishati safi utaendelea kutekelezwa kwa awamu mbalimbali, huku vikundi vya wajasiriamali, mashule, na taasisi za kijamii vikipewa kipaumbele katika mgao wa vifaa hivyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    August 07, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WILAYANI LONGIDO WALA KIAPO CHA UADILIFU

    August 05, 2025
  • SHIRIKA LA MONDO TANZANIA LAKABIDHI MAGODORO 32 KWA WANANFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU SHULE YA MSINGI LONGIDO

    July 30, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • View All

Video

LONGIDO YASHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE MAONESHO YA NANE NANE YANAYOFANYIKA VIWANJA VYA THEMI - NJIRO ARUSHA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.