• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO AWATAKA WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUTUNZA VIFAA NA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Posted on: December 5th, 2024

Shemzigwa: "Tunzeni Vifaa, Fanyeni Kazi kwa Uadilifu"!.


Wilaya ya Longido imehitimisha siku ya pili ya mafunzo ya uandikishaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata. Mafunzo haya yameandaliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa lengo la kuwawezesha wasimamizi hao kutekeleza majukumu yao kwa umakini na weledi.


Akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Nassoro Shemzigwa, alitoa wito kwa washiriki kutunza vifaa watakavyokabidhiwa na Tume, akisisitiza kuwa vifaa hivyo ni muhimu kwa kufanikisha zoezi hilo. "Tutunze vifaa hivi kama mali ya taifa, na zaidi, tufanye kazi kwa kufuata sheria na taratibu tulizoelekezwa. Lengo letu ni kuhakikisha kila mwananchi mwenye sifa anapata nafasi ya kujiandikisha," alisema Shemzigwa.


Aidha, Mwenyekiti wa mafunzo hayo, Bw. Terevaeli Mbise aliipongeza Tume Huru ya Uchaguzi kwa juhudi zake za kuhakikisha mafunzo haya yanafanyika kwa kiwango cha juu. “Mafunzo haya ni muhimu sana kwa wasimamizi wa ngazi ya kata. Tumejifunza mengi na tunaahidi kuyatekeleza kwa ufanisi wa hali ya juu ili kuhakikisha kila mkazi wa kata husika anashiriki kikamilifu katika zoezi hili muhimu,” alisema.


Kwa upande wake, Afisa mwandikishaji  ngazi ya jimbo Bw Nevilling Lymo aliwashukuru washiriki kwa bidii waliyoonyesha katika mafunzo hayo. Alisema kuwa juhudi walizoweka ni ishara ya dhamira yao ya kuhakikisha zoezi linafanikiwa. "Napenda kuwapongeza kwa kujifunza kwa moyo wote. Maarifa haya ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha uboreshaji wa daftari unafanyika kwa usahihi na uwazi," aliongeza.


Washiriki wa mafunzo hayo walieleza kuridhishwa na mafunzo waliyopokea, wakisema kuwa yamewaongezea maarifa muhimu ya kutekeleza majukumu yao kwa umakini mkubwa.


Mafunzo haya ni sehemu ya maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, hatua muhimu kuelekea chaguzi zijazo. Hii ni juhudi ya kuhakikisha kuwa demokrasia ya nchi inaimarika kwa kuwapa wananchi fursa ya kushiriki kikamilifu katika maamuzi ya kitaifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    August 07, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WILAYANI LONGIDO WALA KIAPO CHA UADILIFU

    August 05, 2025
  • SHIRIKA LA MONDO TANZANIA LAKABIDHI MAGODORO 32 KWA WANANFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU SHULE YA MSINGI LONGIDO

    July 30, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • View All

Video

LONGIDO YASHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE MAONESHO YA NANE NANE YANAYOFANYIKA VIWANJA VYA THEMI - NJIRO ARUSHA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.