• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

MKUU WA WILAYA MHE NURDINI BABU AFUNGUA MAFUNZO YA TASAF II AWAMU YA TATU LONGIDO

Posted on: August 10th, 2021

Leo Tarehe 10-08-2021Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe Nurdin Babu amefungua mafunzo ya kuibua kaya maskini kwa wawezeshaji ngazi ya Vijiji kwenye mpango wa TASAF II awamu ya III unaotarajia kufanyika baada ya mafunzo hayo kwa Vijiji ambavyo havikuwepo kwenye mpango huo wa kunusuru kaya maskini Mafunzo hayo pia yanayofanyika katika ukumbi wa Halmashauri umehudhuriwa na Madiwani kutoka kata husika, kamati ya ulinzi na usalama wilaya na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri.

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe Nurdini Babu, wakati wa akifungua Mafunzo iliyohusisha wawezeshaji, watakaokwenda kuzibaini kaya masikini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini mpango wa pili wa TASAF awamu ya tatu, pamoja na waheshimiwa madiwani, timu ya menejimenti ya halmashauri hiyo, semina iliyofanyika kwenye viwanja vya halmashauri ya Longido.

Mkuu wa wilaya Mhe.Nurdin Babu aliwataka wawezeshaji watakaoenda kufanya kazi ya kuibua Kaya masikini kupitia mradi wa kipindi cha pili TASAF awamu ya III, wametakiwa kufanyakazi hiyo kwa weledi na uaminifu mkubwa, ili kuwapata walengwa wenye sifa na vigezo vilivyoaainishwa, kaya ambazo zinakabiliwa na lindi la umasikini uliokithiri, ili kufikia malengo ya serikali ya kupambana na adui umasikini kwa maendeelo ya Taifa la Tanzania.

Mhe Nurdini Babu, amewasisitiza kuwa, wawekezaji hao wameaminiwa na serikali na kuwakabidhi jukumu la kwenda vijijini kubaini kaya masikini zitakazoingizwa kwenye mpango wa ruzuku za TASAF, hivyo wanao wajibu wa katumia fursa vizuri na kwa uadilifu mkubwa, wakiweka uzalendo mbele kwa kufuata vigezo na taratibu zilizowekwa na serikali kupitia TASAF vya kubaini kaya hizo, huku akiwataka waheshimiwa madiwani kutumia majukwaa yao, kuwaeleimisha wananchi sifa na wajibu wa walengo katika mradi huo uliotolewa na serikali katika maeneo yao.

Aidha, Mkuu wa Wilaya, amefafanua kuwa, lengo la kuendeleza mradi huu ambao tayari, ulifanya vizuri katika awamu ya kwanza, serikali imeona ni vyema kuendelea na mradi huo kwa awamu ya pili, na kuzifikia kaya masikini na zenye sifa katika vijiji vyote vya halamshauri na nchi nzima, lengo likiwa ni kuziwezesha kaya hizo, kujikwamua kiuchumi kwa kutumia fursa za kujiongezea kipato, huduma za jamii na kuwekeza katika kuendeleza watoto, pamoja na kuondokana na lindi za umasikini uliokithiri kwa maendeleo ya familia, jamii na taifa kwa ujumla.

Naye Mwenyekiti wa halmshauri ya Longido, Mhe. Simion Oitesoi, amesema kuwa, zoezi la kubaini kaya masikini, ni zoezi la msingi mno, katika halmashauri ya Longido, kutokana na ukweli kwamba kaya nyingi hususani kwenye maeneo ya vijijini ziko katika hali mbaya kiuchumi, zikikabiliwa na changamoto za kuendesha maisha na kushindwa kumudu hata kupata mlo mmoja kwa siku na kuwataka waheshimiwa madiwani wote kuhakikisha wanahamasisha wananchi kupitia mikutano mbalimbali inayofanyika kwenye maeneo yao ili wananchi wajitokeze kwa wingi ili zoezi lifanikiwe kama ilivyokusudiwa pia kuwasaidia wananchi kuibua miradi itakayokuwa na tija kwa jamii zetu.

Mhe Simion Oitesoi  alisisitiza kuwa "Nina wasihi wawezeshaji wote, tambueni kuwa kazi hii mmepewa ni dhamana ya maisha ya watu, serikali imewaamini, hakikisheni mnaifanya kwa uadilifu na kwa kuzingatia haki, kila mmoja wenu ahakikishe anabaini na kuandikisha kaya zenye sifa ya umasikini uliokithiri na si vinginevyo, kaya ambazo zina uhitaji mkubwa wa kusaidiwa na serikali ili waweze kujikwamua lakini pia waheshimiwa madiwani tambueni mna wajibu wa kuwaelimisha wananchi wenu, kuifahamu vizuri TASAF na mradi huu wa kaya masikini pamoja na wajibu wa walengwa katika mradi huo wa TASAF, tumieni mafunzo haya kuwaelimisha wananchi wenu ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima".

"Ninaipongeza serikali ya awamu ya sita, kwa kuona umuhimu wa kuzifikia kaya masikini kwenye vijiji vyote vya halmashauri, hali ambayo licha ya kuwezesha kaya hizo kujimudu kiuchumi lakini itapunguza malalamiko yaliyokuwepo kwa serikali, kupitia mafunzo haya, mimi na madiwani wenzangu, tuna jukumu lamkuelimisha wananchi wetu, waufahamu mradi huu wa TASAF, sifa za kaya zinazohitajika pamoja na wajibu wa kaya masikini katika miradi hiyo ya TASAF" Amefafanua Mheshimiwa Simon.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa TASAF Makao Makuu, Bi Nuru mwezeshaji ngazi ya kitaifa, ameweka wazi sifa za walengwa watakoandikishwa katika kipindi cha pili cha mradi wa TASAF awamu ya tatu kaya zenye kipato cha chini sana na si cha uhakika,kaya ambazo haziwezi kumudu milo mitatu kwa siku, kaya inayoishi kwenye makazi duni, kaya ambayo inawatoto lakini hawaendi shule na kaya ambayo inawatoto wengi hivyo kushindwa kumudu gharama za mahitaji.

Aidha Bi Nuru amefafanua kuwa, licha ya kuwa mradi huu,utatoa ruzuku ya fedha kwa kaya masikini lakini pia kutakuwa na miradi ya kutoa ajira ya muda kwa walengwa, ambapo kaya itataikiwa kuandikisha watu wawili kufanya ajira za muda, lengo likiwa ni kuongezea kaya kipato pamoja na kuwaongezea ujuzi kupitia kazi husika.

Hata hivyo wawekezaji hao 28, wameonyesha ari ya kufanya kazi hiyo kwa umahiri na umakini mkubwa huku wakiweka mbele maslahi ya Taifa, kupitia weledi na uzalendo, kwa maendeleo ya kaya masikini ili waweze kutumia fursa hiyo kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini uliokithiri.

Awali, katika kipindi cha pili cha mradi wa TASAF awamu ya pili, ulizinduliwa rasmi mwaka 2020 mpaka 2023, na unategemea kutumia kiasi cha shilingi trilioni 2.3 na kutekelezwa katika halmashauri 184 za Tanzanzia Bara na visiwani, na kufika jumla ya kaya milioni milioni moja na laki nne na nusu, zenye jumla ya watu milioni saba kote nchini, huku halmashauri ya Longido, ukitegemea kutekelezwa katika kata 18 na vijiji 56.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WILAYA YA LONGIDO WATOA TAMKO JUU YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 23, 2025
  • WANAFUNZI 5,188 KUFANYA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE LONGIDO

    October 21, 2025
  • WWF YADHAMIRIA KUREJESHA MAZINGIRA ASILIA YA LONGIDO

    October 20, 2025
  • MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA PILI YA MAFUNZO YA WWF KWA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA LONGIDO

    October 16, 2025
  • View All

Video

KAMATI YA AMANI NA HAKI WILAYANI LONGIDO YATOA TAMKO LA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.