• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WAILAYA YA LONGIDO MHE.SALUM KALLI AMESHIRIKI ZOEZI LA UGAWAJI WA DAWA ZA KINGA TIBA KATIKA KATA YA KIMOKOUWA WILAYANI LONGIDO.

Posted on: September 30th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli, leo tarehe 30 Septemba 2024, ameshiriki zoezi la ugawaji wa dawa za kingatiba dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza, kama vile trakoma na vikope, katika kata ya Kimokouwa, wilayani Longido. Halmashauri ya Wilaya ya Longido, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na wadau mbalimbali, imeendelea na mpango wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele kama vile minyoo ya tumbo, kichocho, vikope, usubi, na mabusha.

Magonjwa haya yamekuwa yakiathiri jamii, hasa zile zenye kipato cha chini na zinazokaa kwenye maeneo yenye upatikanaji mgumu wa huduma za afya. Mradi wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele umegawanyika katika sehemu mbili. Kwanza, utoaji wa dawa za minyoo na kichocho kwa watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 14, na pili, utoaji wa dawa za vikope kwa watu wote isipokuwa watoto chini ya miezi sita, wajawazito, na wagonjwa mahututi.

Mratibu wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele wilayani Longido, Dk. Felix Mbise, akisoma taarifa ya umezeshwaji wa dawa za vikope, amesema kuwa mwaka 2022, zoezi la utoaji dawa kwa watoto lilifanikwa kwa asilimia 97.1, huku kwa watu wazima likifikia asilimia 88.6. Mwaka huu 2024, awamu ya kwanza imewafikia watoto 30,456 wenye umri wa miaka 5-14, huku watu wazima walengwa wakiwa ni 181,720. Awamu ya pili inatarajiwa kuwafikia walengwa 212,176, na zoezi la umezeshwaji wa dawa bado linaendelea kwenye kata zote wilayani Longido.

Akizungumza na wakazi wa kata ya Kimokouwa, Mheshimiwa Kalli amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi ili kumeza dawa hizo za kingatiba kwa manufaa ya afya zao na jamii kwa ujumla. "Niwaombe ndugu zangu tujitokeze kwa wingi kushiriki zoezi hili kwa ajili ya afya zetu. Bila kuwa na afya njema, huwezi kushiriki shughuli zozote za kimaendeleo, hivyo tuzilinde afya zetu," alisema Mheshimiwa Kalli.

Kwa upande wake, kiongozi wa kimila wa jamii ya Kimaasai, Laigwanani Ngulupa, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwapatia dawa za kingatiba dhidi ya trakoma na vikope, magonjwa ambayo yamekuwa yakiwasumbua wafugaji, hususan katika maeneo yao ambako magonjwa haya huenea kupitia wadudu kama inzi. "Ninamshukuru sana Mkuu wa Wilaya ya Longido kwa kuja kwenye boma letu na kugawa kingatiba dhidi ya trakoma. Nawaomba wananchi wenzangu kujitokeza na kumeza dawa hizi kwa afya zetu," alisema Mzee Ngulupa.

Umezeshwaji wa dawa za Trakoma na vikopr ni zoezi endelevu kwa wananchi na wakazi wa Longido.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM