• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

SIKU YA PILI YA ZIARA YA MKUU WA MKOA WA ARUSHA WILAYANI LONGIDO.

Posted on: November 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa Arusha Mheshimwa John Mongella ameendelea na ziara yake Wilayani Longido ikiwa ni muendelezo wa ziara yake Wilayani humo iliyoanza tarehe 7/11na kukamilika tarehe 8/11.

Mkuu wa Mkoa ametembelea mradi wa ujenzi wa shule mpya Mundarara, amewataka viongozi wa wilaya kufanya hima na jitihada za kukamilisha mradi huo ili wanafunzi waweze kuanza masomo na kuyatumia majengo hayo.

Mheshimiwa ametembelea mradi wa ujenzi  ya Kituo cha Afya Leremeta kilichopo kwenye Kata ya Sinya Wilayani Longido,

Akizungumza na wakazi wa kata hiyo Mheshimwa Mkuu wa Mkoa ametoa salamu zake za dhati kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa amewaona na amesikia kilio chao na yuko tayari kutatua matatizo yao ikiwemo  Zahanati shule, miundo mbinu kama barabara, madaraja.

Pia Mkuu wa Mkoa amemuagiza  Kaimu Mganga Mkuu Daktari Matthew Majani kukamilisha mradi huo ifikapo tarehe 8/12/2023, Sambamba na kupeleka wahudumu katika kituo hicho.

Vile vile ametoa pongezi kwa wananchi wa kata ya Kamwanga alipotembelea ujenzi wa shule kwa Mradi wa Boost ambao umegharimu kiasi cha shilingi Milioni 112 ujenzi wa shule mpya ya Kamwanga kwa Mradi wa SEQUIP ambao Serikali imetoa jumla ya shilingi Milioni 500, ujenzi wa shule mpya ya Irkaswa mradi unazaidi ya milioni 600, pamoja na madarasa ya awali shule ya Irkaswa.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameitaka jamii kufahamu miradi mbali mbali inayofanyika kwenye jamii yao na kuchangia kuitunza na kutoa michango yao pale inapohitajika kwenye ukamilishaji.

"Niwapongeze sana watu wa Kamwanga kwa kuonesha mna muamko mkubwa sana juu ya mambo yanayoendelea katika nchi yetu hasa kwa hizi pesa nyingi zinazotolewa na Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo yale yanayowastaili zikiwemo shule ambazo zitasaidia sana watoto kutotembea umbali mrefu kufuata shule ilipo, ujenzi wa shule hii mpya ya Kata ya Kamwanga ambayo Serikali imetoa zaidi ya milioni 500 kutekeleza mradi huo".Alisema Mkuu wa Mkoa.

Nao wakazi wa Kamwanga wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwaletea maendeleo makubwa kwenye kata yao"Tunamshuru sana Rais kwa kutukumbuka mana sasa tunayo maji, tunazahanati japo bado zinachangamoto, tuna umeme, japo haujafika kwenye vijiji vyote, tuna barabara amabayo tunaomba utekelezaji wa barabara ya Longido-Kamwanga-hadi Rombo Tarakea ili itusaidie kwa shughuli mbali mbali"Alisema ndugu Sara Lemayani mkazi wa Irakaswa.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Longido mheshimiwa Marco Henry Ng'umbi amemshukuru sana Mheshimwa Rais kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi hiyo ya shule Zahanati na Barabara, pia amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuja na kukagua miradi hiyo ya maendeleo kwa ziara hii inasaidia sana kuhimiza ukamilishwaji wa miradi. Sambamba na hilo Mheshimiwa Ng'umbi amewashukuru sana wananchi wa Kamwanga kwa nguvu kazi na michango yao katika kuleta Maendeleo kwenye kata yao."Niwashukuru sana watu wa Kamwanga kwa kujitoa kwenu na utulivu wenu katika kutekeleza na kukamilisha miradi hii"Alisema Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya.

Ziara hizi za mkuu wa Mkoa kwenye miradi ya maendeleo ni ziara endelevu ambazo zinafanyika mara kwa mara kutimiza ilani ya Chama cha Mapinduzi kwenye kuleta Maendeleo ya wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KAZI IENDELEE

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WILAYA YA LONGIDO WATOA TAMKO JUU YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 23, 2025
  • WANAFUNZI 5,188 KUFANYA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE LONGIDO

    October 21, 2025
  • WWF YADHAMIRIA KUREJESHA MAZINGIRA ASILIA YA LONGIDO

    October 20, 2025
  • MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA PILI YA MAFUNZO YA WWF KWA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA LONGIDO

    October 16, 2025
  • View All

Video

KAMATI YA AMANI NA HAKI WILAYANI LONGIDO YATOA TAMKO LA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.