• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIFO VYA UZAZI WA AKINA MAMA NA WATOTO VINAWEZA KUISHA, DC

Posted on: June 20th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Longido chini ya Mkurugenzi Mtendaji Ngd. Jumaa Mhina kupitia Idara ya Afya wameendelea kushirikiana vyema na wataalamu wa Afya ngazi ya Mkoa kwa kuahakikisha wanapunguza na hata kumaliza kabisa vifo vya Uzazi wa akina Mama na watoto.

Akifungua kikao cha kampeini yenye kauli mbiu isemayo “JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA” na maneno ya “Maneno sasa basi, Vitendo tu! Jiongeze! Tuwavushe salama. Mama mjamzito akivuka salama Mtoto atakuwa salama, Familia itavuka salama na Nchi itakuwa salama” Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe. Frank James Mwaisumbe asubuhi ya Juni 20,2019 katika ukumbi wa Halmashauri ya Longido amesema kuwa vifo vya uzazi wa akina Mama na watoto vinaweza kuisha kabisa kama tu wahusika wote watawajibika ipasavyo.

Aidha Mhe. Mwaisumbe ameeleza kuwa Serikali inatambua uwepo wa changamoto za ukosefu wa miundombinu ya Afya ikiwemo Vituo vya Afya, barabara, magari, maji n.k na ndio maana imekwishaanza kuchukua hatua za haraka kwa kuwajengea kituo kikubwa cha Afya ambayo ni Hospitali ya Wilaya na inatarajiwa kukabidhiwa mwishoni mwa mwezi juni, kuwaletea mradi mkubwa wa maji ambao umekwishaanza kusambaza maji ndani ya Longido pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara na umeme.

Mapema kabla ya ufunguzi wa kampeini hiyo Mkurugenzi mtendaji Ndg.Jumaa Mhina amesema kuwa Longido sasa ni kitovu cha maendeleo kwani ni miongoni mwa Wilaya ambazo zinaendelea kupewa kipaumbele na Serikali ya Dk. John Magufuli kwa kuboresha miundombinu.

Naye mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dk.Wedson Sichwalwe amefafanua jitihada za maksudi za Kupunguza na kumaliza kabisa vifo hivyo zinaonekana kwani kipindi cha Januari-Machi 2019 akijatokea kifo chochote cha uzazi wa Mama na Mtoto katika Mkoa wa Arusha.

Justice Eliangao Munisi Mganga mkuu wa wa Wilaya Longido amema kuwa kupungua kwa vifo hivyo kumechangiwa na kampeini za mara kwa mara za kuongeza uwajibikaji wa wataalamu katika kuzuia vifa vya Mama na Watoto.

Hata hivyo amebainisha kuwa zipo changamoto kama ubovu wa miundombinu, ukosefu wa magari ya wagonjwa,wazazi kutokwenda ama kuchelewa kufika kujifungulia katika vituo vya Afya. Vilevile amesema kuwa njia zitakazoendelea kusaidia kutatua vifo hivyo ni pamoja na dawa za kuzuia kifua cha mimba,wataalamu kutoa mabaka ya uzazi pamoja na kusaidia mtoto mchanga ambaye hana nguvu mara baada ya kuzaliwa.

Katibu wa Afya Wilaya ya Longido Josia Mruve amesema sasa Longido imepiga hatua kubwa katika kutoa Elimu kwa wananchi kwani kwa mwaka 2017 akina Mama waliojifungulia kituo cha Afya ni 21% na katika kipindi cha Januari- Mach 2019 waliojifungulia katika vituo vya Afya ni 51%.

 Kikao hicho kimehhudhuliwa na Wataalamu wa Afya kutoka Mkoani Arusha, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido …………………………….,wanaharakati wa Afya Wilaya ya Longido pamoja na viongozi wa kimila.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM