• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WADINI WAKABIDHI SADAKA KWA WATOTO WANAOISHI NYUMBA SALAMA WILAYANI LONGIDO

Posted on: January 22nd, 2025

Na Happiness Nselu


Longido, 22 Janauri 2025 – Watoto wanaoishi katika kituo cha nyumba salama Wilayani Longido wamenufaika na msaada wa sadaka kutoka kwa viongozi wa dini na wananchi,Sadaka hizo zimewasilishwa na viongozi hao walipowatembelea watoto hao katika kituo hicho cha nyumba salama kilichopo wilayani humo mnamo tarehe 21.01.2025. Sadaka zilizowasilishwa zilitolewa wakati wa dua ya kuiombea wilaya na taifa iliyofanyika tarehe 28.12.2024,Dua iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli.

Akizungumza katika tukio hilo, Mwenyekiti wa Viongozi wa Dini wa Wilaya ya Longido, Shekhe Ramadhani Mpangala, alikabidhi sadaka hizo kwa niaba ya wananchi wa wilaya. Shekhe Mpangala alisisitiza umuhimu wa kujitolea na mshikamano kwa ajili ya watoto wanaoishi katika nyumba salama, ambao wanahitaji msaada wa kila aina ili kukabiliana na changamoto za maisha. Alisema msaada huo ni muhimu katika kuhakikisha watoto hao wanapata mahitaji ya msingi ambayo ni nguzo muhimu katika kukuza na kuimarisha maisha yao.

Mchungaji Aidan Mwikolla, ambaye pia alizungumza kwa niaba ya viongozi wa dini, aliwataka wananchi na wadau mbalimbali kujitokeza kwa wingi kutoa msaada kwa watoto hao. Alieleza kuwa msaada huo unajumuisha vitu muhimu kama nguo, chakula, madaftari, na vifaa vya shule, ambavyo vitasaidia watoto hao kuendeleza masomo yao na kuwa na maisha bora. Aliongeza kuwa kutoa sadaka kwa watoto hawa ni jukumu la kila mmoja katika jamii, kwani watoto ni hazina ya taifa.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Longido na Kamati ya Usimamizi wa Nyumba Salama, Bw. Omary Ramadhani, alitoa shukrani kwa viongozi wa dini na wananchi waliotoa sadaka zao. Alisema kuwa msaada huo ni muhimu hasa kwa watoto wanaoishi katika nyumba salama, ambapo wengi wao wanategemea msaada wa jamii kwa ajili ya kuendelea na masomo na maisha yao ya kila siku. Aliwashukuru wananchi kwa kujitolea na kuwataka kuendelea kuwasaidia watoto hawa ili waweze kupata mahitaji yao ya msingi, kwani wapo wanafunzi wengi ambao wanategemea msaada huu ili kuweza kufanikiwa katika masomo yao.

Afisa Ustawi wa Wilaya, Bw. Abdalah Nyange, ambaye alikabidhi msaada kwa niaba ya watoto, alitoa shukrani kwa viongozi wa dini, ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya, na wananchi kwa msaada wao endelevu. Bw. Nyange alitoa wito kwa jamii kuendelea kuwasaidia watoto hawa, huku akisisitiza kuwa bado mahitaji ni makubwa. Alitoa wito pia kwa jamii kuacha vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na kuhakikisha familia zinazingatia malezi bora ya watoto kwa upendo. Aliitaka jamii kuwa na moyo wa huruma na kutoa msaada bila kutarajia malipo ili kuleta mabadiliko chanya kwa watoto hao.

Hafla hiyo ilionyesha mshikamano wa kipekee wa wananchi wa Longido katika kusaidia watoto wanaoishi nyumba salama, huku viongozi wa dini na wadau mbalimbali wakitumia fursa hiyo kutoa wito wa kuendeleza msaada kwa watoto hao na kuhakikisha wanapata maisha bora na ya kimaendeleo. Viongozi hao walisisitiza kuwa msaada wa jamii ni muhimu ili watoto hawa waweze kufikia ndoto zao na kuwa raia bora wa taifa la kesho.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LONGIDO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA MAFANIKIO MAKUBWA

    August 07, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WILAYANI LONGIDO WALA KIAPO CHA UADILIFU

    August 05, 2025
  • SHIRIKA LA MONDO TANZANIA LAKABIDHI MAGODORO 32 KWA WANANFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU SHULE YA MSINGI LONGIDO

    July 30, 2025
  • LONGIDO YANG'ARA KITAIFA YAPATA TUZO YA UFAULU KIDATO CHA PILI

    July 11, 2025
  • View All

Video

LONGIDO YASHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE MAONESHO YA NANE NANE YANAYOFANYIKA VIWANJA VYA THEMI - NJIRO ARUSHA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.