• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Fedha, Utawala na Mipango

KAMATI YA FEDHA, UTAWALA NA MIPANGO

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ni moja ya Kamati za kudumu za Halmashauri na  inaundwa kwa kushirkisha Wenyeviti wa Kamati za Kudumu na hukutana mara moja kila mwezi na moja ya majukumu yake ya Msingi ni pamoja na kusimamia na kudhibiti ukusanyaji wa mapato na matumizi ya mali za Halmashauri kupitia Vikao vyake. Majukumu mengine ni;

Kuweka mikakati na kupendekeza uongezaji wa mapato

Kuwasilisha mapendekezo ya bajeti na Mpango wa Maendeleo wa Halmashauri ili kuidhinishwa na Halmashauri

Kusimamia utunzaji wa fedha ikiwa ni pamoja na kufuta madeni, kuhakiki mali za Halmashauri, kuomba vibali maalum kwa matumizi yanayohitaji kibali cha Waziri mwenye dhamana

Kufikiria na kupendekeza mabadiliko ya viwango vya kodi, ada na ushuru mbalimbali vinavyotolewa na Halmashauri

Kushughulikia orodha ya wadaiwa wote itakayowasilishwa kwenye Kamati na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua

Kujadili na kupendekeza masuala yote yanayohusu maslahi ya jumla ya Watumishi ikiwa ni pamoja na kuthibitisha Watumishi kazini, mikopo, nyumba, usafiri, matibabu, rambirambi, masomo na motisha nyinginezo

Kupokea na kuzingatia mapendekezo ya kubadili matumizi ya mafungu ya fedha yaliyopo kwenye makisio (reallocation) na kuyawasilisha kwenye Halmashauri

Kuratibu mapendekezo kutoka kwenye Kamati nyingine kuhusu matumizi ya kawaida na miradi na kuyawasilisha kwenye Halmashauri

Kufikiria na kupendekeza kwenye Halmashauri kuhusu Mikopo yote ya Halmashauri

Kutoa mapendekezo ya vitega Uchumi kwa madhumuni ya kuongeza mapato kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura ya 290

Kupokea na kujadili Taarifa za Wakaguzi wa Fedha na mali za Halmashauri na kupendekeza hatua za kuchukuliwa kutokana na maelekezo na maoni ya Wakaguzi kwa mujibu wa Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Sura ya 290

 Kupokea na kudhibiti matumizi ya fedha za Halmashauri kwa kuzingatia Taratibu zilizowekwa na Waziri na nyingine zitakazowekwa na Halmashauri

Kupitia marekebisho yote yaliyopendekezwa hususan kuhusu taratibu za fedha ikiwa ni pamoja na mapitio ya mara kwa mara yanayohusu thamani ya fedha ambapo Kanuni mbalimbali za Manunuzi ya mali na Vifaa hutumika.

Kushughulikia tofauti ya Mapato na Matumizi kwenye Bajeti na kupendekeza hatua stahili za kuchukua

Kupokea na kujadili Taarifa za Fedha kila mwezi na Robo mwaka

Kushughulikia Sera kuhusu kukopa na Uwekezaji

Kubuni na kupendekeza mpango wa kuanzisha na kuendeleza uhusiano na Halmashauri nyingine

Kurekebisha na kusimamia makusanyo na matumizi ya Mapato ya Vijiji kwa mujibu wa Sheria Sura ya 287

Kuteua Wakaguzi wa Fedha/Mali za Serikali za Vijiji kwa mujibu wa Sheria, Sura ya 290

WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA, UTAWALA NA MIPANGO KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019

NA

JINA

KATA

CHAMA

1
MHE. SABORE K. MOLLOIMET
M/KITI WA HALMASHAURI - MWENYEKITI
CCM
2
MHE. ESUPAT K. NGULUPA
MAKAMU MWENYEKITI – VITI MAALUM
CCM
3
MHE. ALAIS MUSHAO
M/KITI WA KAMATI YA ELIMU, AFYA & MAJI
CCM
4
MHE. PETER LEKANETI
M/KITI WA KAMATI YA UCHUMI, UJENZI & MAZINGIRA
CCM
5
MHE. PETER NDEREKO
M/KITI WA KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
CCM
6
MHE. DR STEPHEN KIRUSWA
MBUNGE
CCM
7
MHE. MOTIKA KASOSI
ORBOMBA
CCM
8
MHE. SARA OLTETIA
VITI MAALUM – MUNDARARA
CCM
9
MHE. JOPHA KAKANYI
VITI MAALUM – ENGARENAIBOR
CCM
10
MHE. UPENDO MTAGWA
VITI MAALUM – LONGIDO
CHADEMA
11
MHE. TIMOTHEO MONYORIT
KETUMBEINE
CCM
12
MHE. SIMON OITESOI
GELAI LUMBWA
CCM

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM