• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MWL. NYERERE FOUNDATION YAWEKA KAMBI YA SIKU MBILI WILAYANI LONGIDO WAKIHUBIRI AMANI , UMOJA NA MAENDELEO YA WANANCHI

Posted on: January 16th, 2020

Taasisi ya Mwalimu Nyerere iliweka kambi wilayani Longido kwa siku mbili kwa lengo la kuhamasisha umuhimu wa watanzania kutunza Amani na umoja ambazo ndio nguzo ya maendeleo kama Mwl Nyerere alivoagiza kipindi cha uhai wake na ikiwa ni kazi kubwa ya tasasisi hiyo kuhubiri Amani na umoja Tanzania na hata duniani kote.Mkurugenzi mtendaji wa Mwl.Nyerere foundation , Mzee Joseph Butiku alieleza kwa undani na mapana zaidi Nafasi ya viongozi wa ngazi ya serikali za mitaa katika kusimamia katiba , na kuawaeleza viongozi hao ambao ni wenyeviti wa vijiji na watendaji wa kata kua wananchi wanapaswa kusimamiwa kwa mujibu wa katiba na sheria zilizowekwa ili kuepuka migogoro na wananchi na pia viongozi hao wasisite kuwaelimisha wanannchi wao kuhusu umuhimu wa amani katika jamii ili kuwa na jamii salama na yenye kufanya kazi kwa juhudi ili iweze kujipatia maendeleo.

Mzee Gallus Abedi msaidizi maalum wa Mkurugenzi wa Tasisi ya Mwalimu Nyerere pia alizungumzia  juu  ya  namna uongozi wa kijiji , kata , wilaya  , mila na vikundi mbalimbali wanavyopaswa kusimamia Amani , Umoja na Maendeleo ya wananchi akisema kua viongozi wanapaswa kua mstari wa mbele  kuzungumza  habari  ya  Amani  kila wanapokutana  na  wananchi  kwani Amani na umoja wa wananchi hao utawapa nafasi ya kufanya kazi kwa pamoja na ushirikiano hivyo watakua na nafasi ya kuendelea, Mzee Abedi pia alisisitiza kua viongozi hao wanapaswa kulinda rasilimali zilizopo na kuzisimamia kikamilifu  rasilimali hizo kama ardhi ili kuepusha migogoro itakayochochea upotevu wa amani katika jamii wanazo zisimamia kama viongozi.   Mwisho wazee  hawa  kutoka Taasisi ya mwalimu Nyerere walishauri  serikali  hasa  Halmashauri ya Wilaya ya Longido  kushuhulikia  mambo yanayowahusu Wananchi wa Wilaya hiyo bila kuchelewa  hasa  mambo yanayohusu mipaka na umiliki wa ardhi ili kuepusha upotevu wa Amani kwenye jamii ya watu wa Longido. Ikiwa kama dhumuni la taasisi hiyo kuhubiri Amani, umoja na maendeleo ya wananchi , Uongozi wa wilaya ya longido uliwashukuru Taasisi hiyo na kuahidi kufanyia kazi ushauri na maelekezo ya wazee hao wa Taifa la Tanzania na Taasisi ya Mwl .Nyerere.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM