• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu,Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mijinii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Usafishaji na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Maliasili na Utalii
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Rasilimali Asili na Hifadhi ya Mazingira
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasili na uhifadhi wa mazingira
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Leseni
    • Mapato
    • Utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,Afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti UKIMWI
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Huduma zetu-Utalii

 Wilaya ya Longido ni miongoni mwa wilaya sita (06) za Mkoa wa Arusha, kaskazini mwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jina “Longido” limetokana na Mlima Longido, ambao kwa lugha ya Kimasai huitwa Loongiito, likimaanisha “mlima wenye mawe ya kunolea visu.” Wilaya hii ina eneo la kilomita za mraba 8,180.

Kijiografia, Wilaya ya Longido imezungukwa na mifumo mikubwa ya ikolojia inayochangia umuhimu wake kama mazalia, malisho na mapito ya spishi mbalimbali za wanyamapori. Upande wa mashariki inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA) iliyounganishwa na Ushoroba wa Kimataifa wa Kitenden (Kitenden Wildlife Corridor). Kusini inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Arusha (ANAPA), magharibi na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) pamoja na Pori la Akiba la Pololeti, huku kaskazini ikipakana na Hifadhi ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya.

Mbali na mandhari yake ya kipekee, Wilaya ya Longido imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, vikiwemo spishi zaidi ya 40 za wanyamapori, aina mbalimbali za ndege wakiwemo Heroe wadogo (Lesser Flamingo) wenye mazalia Ziwa Natron, Mbuni (Ostrich), Tandawala (Kori Bustard) na Ndege Sekretari (Secretary Bird) pamoja na urahisi wa kufikika maeneo mengi ya vivutio. Mchanganyiko huu wa rasilimali na fursa unaiweka Longido katika nafasi ya kipekee kama kitovu cha shughuli za utalii kaskazini mwa Tanzania.

        Jedwali Na.1. Baadhi ya wanyamapori wanaopatikana Wilayani Longido.


Jina la kawaida
Spishi
Tembo
Loxodonta Africana
Nyati
Syncerus caffer
Twiga
Giraffa Camelopardalis
Simba
Panthera leo
Duma
Acinonyx jubatus
Chui
Panthera pardus
Mbwa Mwitu
Lycaon pictus
Digidigi
Madoqua kirkii
Pofu
Tragelaphus oryx
Mbuzi mawe
Oreotragus oreotragus
Swala pala
Aepyceros melampus
Swala Granti
Grant    gazelle
Tandala kubwa
Tragelaphus strepsiceros
Tandala mdogo
Tragelaphus imberbis
Choroa
Fringed Eared Oryx
Mbuni
Struthio camelus
Fisi madoa
Crocuta crocuta
Fisi Mraba
Hyaena hyaena
Swala thomi
Eudorcas thomsonii
Ngiri
Phacochoerus africanus
Nyumbu
Connochaetes taurinus
Pundamilia
Equus quagga
Swala Twiga
Litocranius walleri
Kori Bustard
Ardeotis kori
Heroe wadogo (Lesser Flamingo)
Phoeniconaias minor


Uwindaji wa Kitalii (Tourist Hunting):

Hii ni aina ya uvunaji wa wanyamapori madume yaliyozeeka unaofanywa na Wawindaji Wageni chini ya usimamizi wa Serikali kwa lengo la Utalii (Consumptive Wildlife Utilization). Mgeni anapaswa kulipia ada ya vibali na wanyama kupitia Kampuni inayomiliki Kitalu husika cha Uwindaji kabla ya kusafiri kutoka nchi yake kuja nchini Tanzania kwa Shughuli za Uwindaji. Aina hii ya Uwindaji, inafanyika katika maeneo maalum yaliyotengwa na Serikali kama vitalu vya Uwindaji kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii. Aidha, mwishoni mwa mwaka 2022, Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mnada wa Kielectroni (Electronic Auctions), iligawa Vitalu saba (07) vya Uwindaji Wilayani Longido kwa Kampuni sita (06) za Uwindaji kama inavyosomeka kwenye Jedwali Na.2. hapo chini.

Jedwali Na.2. Orodha ya Vitalu vya Uwindaji Wilayani Longido na Kampuni zinazomiliki. 

 

S/N
JINA LA KITALU
KAMPUNI INAYOMILIKA
MUDA WA UMILIKI

Pori Tengefu Ziwa Natron Kaskazini.
Adam Clements Safaris Ltd.
2023 - 2032

Pori Tengefu Ziwa Natron Kusini.
Robin Hurt Safaris Ltd.
2023 - 2032

Pori Tengefu Ziwa Natron Magharibi.
Kilombero North Safaris Ltd.
2023 - 2032

Pori Tengefu Ziwa Natron Mashariki.
Green Mile Safaris Co. Ltd
2023 - 2042

Pori Tengefu Longido Kaskazini.
Michel Mantheakis Safaris Ltd
2023 - 2032

Monduli Juu Open Area.
Tanzania Big Game Safaris Ltd.
2023 - 2032

Eneo la Uwindaji la Engasurai-EWMA
Kilombero North Safaris Ltd.
2023 - 2032

Utalii wa Picha (Photographic Tourism):

Hii ni aina ya utalii usio wa uvunaji (Non-Consumptive Wildlife Utilization) unaofanywa na wageni kwa kutembelea vivutio vya Utalii ndani ya Wilaya yetu kwa lengo la kupiga picha na kutazama wanyamapori katika mazingira yao. Wageni wengi hufika Longido kutazama Wanyamapori mbalimbali na ndege pamoja na kupanda mlima Longido wenye urefu wa mita 2,637 kujionea mandhari tambarare za mbuga zinazozunguka Mlima Kilimanjaro na Meru.

Utalii wa Kitamaduni (Cultural Tourism): 

Longido ni kitovu cha Utalii wa Kitamaduni ambapo wageni wanaweza kutembelea maboma ya Wamasai kwa Lengo la kujifunza kuhusu mila, tamaduni na maisha ya kila siku ya Jamii ya Wamasai. Wageni wataweza kupata fursa ya kupiga picha ya matukio halisi ya jamii hiyo kama wanawake wakiokota kuni, watoto wakichunga mifugo, na usanifu wa kipekee wa boma za Wamasai (nyumba za makazi).



Kwa maelezo na msaada zaidi fika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Longido, au

 piga simu namba :

 0784889889 Afisa Wanyamapori Wilaya,

 0787115234 Afisa Utalii Longido.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.