• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

VIONGOZI WATEULE NGAZI ZA MITAA, VIJIJI NA VITONGOJI WAMEKULA KIAPO CHA UTII NA UADILIFU MBELE YA HAKIMU SHILA MKOMA.

Posted on: November 27th, 2019

Leo tarehe 27-11-2019 msimamizi mkuu wa uchaguzi wa serikali zavijiji na vitongoji Jimbo la Longido Bi Natang’aduak Zakayo Mollel amelisimamia zoezi nzima la kuwaapisha viongozi mbalimbali vijiji na vitongoji katika ukumbi wa JK Nyerere ulioko hapa Halmashauri ya Longido. Katika zoezi hilo Hakimu mkazi wa mahakama ya mwanzo wilaya  Longido Ndugu Shila Mkoma Dyumu aliwaapisha takribani viongozi 1225 ikiwemo wenyeviti wa vijiji 49,wenyeviti wa vitongoji 176,wajumbe wa kundi mchanganyiko 608 na wajumbe wa viti maalum 392 kutoka katika vijiji na vitongoji mbalimbali wakiwa wanatoka Chama Cha Mapinduzi CCM.

Pia utoaji wa viapo ulishuhudiwa na katibu wa Chama Cha Mapinduzi wilaya Ndugu Ezekiel Mollel, mwakilishi wa mkuu wa wilaya,afisa kupambana na kuzuia Rushwa Takukuru wilaya Ndugu Ally Mikidadi ,mwakilishi wa OCD,viongozi wa dini na wataalam wa idara na vitengo mbalimbali vya Halmashauri.

Bi.Natang’aduaki Mollel alitumia nafasi hii kuwapongeza sana viongozi hao kwa kupata kibali cha kupewa nafasi ya kuwatumikia wananchi kwa kipindi cha miaka minne na kuwataka waende wakatatue kero mbalimbali za wananchi na kufanya kazi kwa uadilifu na utii bila upendeleo wowote. Pia alitoa shukrani kubwa sana kwa ushirikiano alioupata kutoka kwa watendaji mbalimbali kabla na wakati wa uchaguzi kwani zoezi la uchaguzi lilienda vizuri hakukua na vitendo vyovyote vya kuonewa, kupendelewa na uvunjivu wa amani.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya Longido Ndugu Ezekiel Mollel pia aliwapongeza viongozi hao wateule kwa kupata dhamana ya kuwaongoza wananchi na kuwataka waende kuwatumikia wananchi na kutatua kero ambazo zinawafanya wananchi kuichukia na kutoipenda CCM ili kukifanya chama kiweze kukubalika na kupata dhamana tena kwenye chaguzi zijazo. Pia aliwataka kuacha kukisema vibaya chama kwani ndicho kilichowaweka madarakani na kuacha vitendo vya rushwa kwenye kuwatumikia wananchi na kutosita kuwaondoa na kuwafukuza viongozi wazembe kwenye chama.

Mwakilishi wa OCD wilaya pia aliwapongeza viongozi wateule kwa kupata nafasi ya kuwatumikia wananchi na kusema kuwa kutokana na katiba yetu mimi sina chama kazi yangu kubwa ni kuhakikisha wananchi wanafuata sheria bila kulazimishwa endapo itaoneka unavunja sheria basi tunakukamata. Pia aliwataka viongozi waende kusimamia ulinzi na usalama kwenye maeneo yao kwa kuanzia kamati ya ulinzi na usalama katika maeneo wanayoyaongoza na kukemea vitendo viovu ikiwemo rushwa, ndoa za utotoni na wahamiaji haramu.

Afisa wa Kuzuia na Kupambana na Rushwa Ndugu Ally Mikidadi aliwapongeza viongozi wateule na kuwaambia kuwa leo mmekuja kula kiapo maana yake ni kwamba unaingia mkataba na serikali hivyo basi ukikutwa na kosa lolote lile uko tayari kushtakiwa kulingana na sheria na taratibu za nchi. Pia aliwataka viongozi wakawe mabarozi wazuri wakukemea na kutokomeza rushwa katika maeneo yao ikiwemo kwenye maswala ya ardhi na kwenye kuwatumikia wananchi kwani rushwa inasababisha vifo na upendeleo kwenye jamii.

Mwisho Bi Natang’aduak alimalizia kwa kuwasihi wenyeviti na wajumbe mbalimbali wakafanye kazi kwa ushirikiano na kuwa mstari wa mbele katika kuwatatulia wananchi kero zao na kuwafichua wale wote wanaofanya vitendo viovu ikiwepo kuwaficha Watoto wanaotakiwa kuanza shule, ndoa za utotoni na ukeketaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.