• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

HESLB YATOA SIFA, UTARATIBU UOMBAJI MIKOPO 2019/2020

Posted on: July 2nd, 2019

HESLB YATOA SIFA, UTARATIBU UOMBAJI MIKOPO 2019/2020

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza mwongozo wa utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 unaotaja sifa, vigezo na utaratibu wa kuwasilisha maombi ya mikopo ya elimu ya juu na kuwasihi waombaji mikopo watarajiwa kuusoma kwa makini na kuuzingatia.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amewaambia wanahabari leo (Jumanne, Juni 4, 2019) jijini Dar es salaam kuwa lengo la kutoa mwongozo huo ni kuwawezesha waombaji mikopo kuandaa nyaraka muhimu zinazotakiwa.

Kwa mujibu wa Badru, HESLB imetoa mwongozo huo kabla ya kufungua mfumo wa maombi ya mkopo ili kuwawezesha waombaji mikopo watarajiwa kuandaa nyaraka muhimu. Mfumo wa maombi kwa njia ya mtandao utafunguliwa Juni 25, 2019 na utafungwa Agosti 15, 2019.

Uzoefu na sababu za kutoa mwongozo
“Uzoefu wetu unaonesha kuwa waombaji wengi hukimbilia kwenye mtandao na kujaza fomu za maombi wakati mwingine bila kusoma mwongozo. Mwaka huu tumetoa mwongozo huu kwanza ili wausome kwa wiki takribani mbili kabla ya kuruhusiwa kuanza kujaza fomu kwa njia ya mtandao,” amesema Badru na kuongeza kuwa katika mwaka 2018/2019, waombaji zaidi ya 9,000 kati ya 57,539 waliokuwa na sifa za msingi walikosea kujaza fomu za maombi.

Ili kutatua tatizo hilo mwaka 2019/2020, Badru amesema HESLB imetembelea shule za sekondari 81 katika mikoa 17 ya Tanzania Bara na Zanzibar na kukutana na wanafunzi 27,489 ambao walielimishwa kuhusu sifa na utaratibu wa kuomba mkopo kwa usahihi.

Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema mwongozo huo unapatikana katika lugha za kiingereza na kiswahili katika tovuti ya HESLB ambayo ni www.heslb.go.tz

“Pamoja na mwongozo huo, pia tumeandaa kijitabu chenye maswali na majibu yanayoelekeza namna ya kuomba mkopo kwa lugha ya kiswahili … nacho pia kinapatikana kwenye tovuti yetu na tunawashauri wakisome,” amesema Mkurugenzi Mtendaji huyo.

Nyaraka muhimu za kuandaa
Waombaji wote wanatakiwa na vyeti vya kuzaliwa ambavyo vimethibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) au Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA). Aidha, kwa waombaji mikopo ambao wazazi wao wamefariki dunia, watatakiwa kuwa na nakala za vyeti vya vifo ambavyo vimethibitishwa na RITA au ZCSRA.

“Vilevile tunafahamu kuwa kuna wanafunzi waliofadhiliwa na taasisi mbalimbali katika masomo yao ya sekondari au stashahada, hawa wanatakiwa kuwa na barua kutoka katika taasisi hizo,” amesema Badru katika mkutano huo uliohudhuriwa na Mkurugenzi wa Upangaji Mikopo wa HESLB Dkt. Veronika Nyahende.

Kwa wanafunzi wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu, Badru amesema wanapaswa kuwa na barua zinazothibitisha ulemavu wao kutoka kwa waganga wakuu wa wilaya au mikoa.

Maeneo muhimu yaliyoboreshwa kwa 2019/2020
Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji huyo aligusia maeneo muhimu yaliyoboreshwa katika utoaji mikopo kwa lengo la kuwafikia wanafunzi wahitaji wengi zaidi.

“Baada ya kupokea maoni ya wadau, tumeongeza umri wa waombaji mikopo kutoka miaka 33 hadi 35 na pia mwaka huu tutapokea maombi kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita au stashahada ndani ya miaka mitano iliyopita … kabla ilikuwa miaka mitatu tu,” amesema Badru.

Malengo na bajeti
Katika mwaka wa masomo 2019/2020, Serikali kupitia HESLB imepanga kutoa mikopo na ruzuku ya elimu ya juu yenye thamani ya TZS 450 bilioni kwa jumla ya wanafunzi 128,285. Kati ya hao, wanafunzi 45,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza. Mwaka huu 2018/2019, unaoelekea mwisho; jumla ya TZS 427.5 bilioni zilitolewa kwa jumla ya wanafunzi 123,000.

Dawati la huduma kwa wateja
Pamoja na mwongozo uliotolewa, dawati la huduma kwa wateja litakuwa wazi ili kutoa ufafanuzi pale utakapohitajika. Wateja wetu pia wanaweza kupiga simu au kutuandikia barua pepe kwa:

Simu: 0736 665533 au 0739 66 55 33 au 022 5507910
Barua pepe: adcp@heslb.go.tz au info@heslb.go.tz

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.